Mwaka jana mwezi wa nane(August),tuliuliza swali katika post hii hapa.Kichwa cha habari kilikuwa katika lugha ya Kiingereza kwamba Dr.Asha-Rose Migiro:The Next President? Swali lile tuliliuliza kufuatia kilichokuwa kikiendelea katika duru za kisiasa wakati ule. Kulikuwa na tetesi kwamba Dr.Migiro,huenda akajitupa ulingoni kuwania Urais mwaka 2015.Wadau mbalimbali wakawa wakiongelea uwezekano wa Tanzania kupata Rais wa Kwanza Mwanamke na mambo kama hayo.
Kwa bahati nzuri au mbaya,wakati ule Dr.Asha-Rose Migiro bado alikuwa akishikilia cheo chake cha U-naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa(United Nations) na hivyo kufanya tetesi zile ziishie hewani kama vile mvuke wa maji ya moto tu. Mambo yamebadilika kidogo hivi majuzi ilipojulikana kwamba Dr.Migiro atakiachia cheo cha U-Naibu Katibu Mkuu wa UN kwa sababu muda wake umemalizika.Haijawekwa wazi kwamba kwanini yeye aondoke wakati Katibu Mkuu wake,Ban-Ki Moon bado yupo na kama walikuwa na ajenda basi ni yao wote kuitekeleza.Anyway,hayo ni mambo mengine,tuyaache kwa sasa.
Sasa kwa sababu Dr.Migiro anaondoka UN na hivyo kumaanisha kwamba atakuwa na nafasi zaidi ya kuwania Urais wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2015, tayari fukuto la maoni ya wananchi limeanza kutanda. Je,agombee mwaka 2015? Je anafaa?Je,Tanzania ipo tayari kwa Rais Mwanamke? Hayo ni baadhi ya maswali yasiyo na majibu ya moja kwa moja ambayo yamekuwa yakisikika iwe ni mtaani,mitandaoni,katika vyombo mbalimbali vya habari hususani Radios nk.Nini maoni yako wewe msomaji wa BC?

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumanne, Novemba 29, 2011, ametia saini Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011.
Hatua hiyo ya Mheshimiwa Rais kutia saini Muswada huo inakamilisha safari ya kutungwa kwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011 baada ya Bunge kuwa limepitisha Muswada huo uliowasilishwa na Serikali katika kikao kilichopita cha Bunge.
Aidha, kutiwa saini kwa Muswada huo ili uwe Sheria ni hatua kubwa na muhimu katika safari ya kutungwa kwa Katiba mpya ya Tanzania kama ilivyoahidiwa na Mheshimiwa Rais Kikwete katika salamu zake za Mwaka Mpya kwa wananchi Desemba 31, mwaka jana, 2010.
Pamoja na kutiwa saini hiyo bado Serikali itaendelea kusikiliza maoni na mawazo ya wadau na wananchi mbalimbali kuhusu namna ya kuboresha sheria hiyo.
Hivyo, Mheshimiwa Rais Kikwete anatoa wito kwa mwananchi yoyote mwenye maoni ama mawazo ya namna ya kuboresha Sheria hiyo, ajisikie yuko huru kutoa maoni yake na Serikali itasilikiza na kuchukua hatua zipasazo.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
29 Novemba, 2011
Rais Jakaya Mrisho Kikwete jioni ya leo tarehe 27 Novemba 2011,amekutana na viongozi wa chama kikuu cha upinzani,CHADEMA,Ikulu jijini Dar-es-salaam ili kuzungumza nao juu ya musuada uliopitishwa hivi karibuni Bungeni kuhusu sheria ya kuundwa kwa tume ya kukusanya maoni ya wananchi juu ya uundwaji wa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kama utakumbuka wabunge wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) walisusia upitishwaji wa musuada huo mjini Dodoma.Hii hapa ni SLIDESHOW ya picha mbalimbali kutoka katika mkutano huo ambao bado haijawekwa wazi juu ya yale yaliyoamuliwa.Lakini kutokana na muonekano wa picha tu,yaelekea ulikuwa mkutano mzuri!
Picha zote na Ikulu.Ukitaka kuiona picha katika ukubwa wake,bonyeza juu yake.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Waziri Mkuu,Pinda.Ingekuwa picha hii imepigwa jana ningesema bila shaka wanafurahia ushindi wa…

Picha na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO

Msomaji mwenzetu mmoja hapo jana aliomba kuona picha ya Baraza la Mawaziri la sasa baada ya kuona picha ya Baraza la Kwanza la Mawaziri baada ya Muungano katika post iliyopo hapo chini inayomzungumzia Oscar Kambona na Wikipedia.
Kwa bahati mbaya,hatuna picha ya Baraza la Mawaziri lililopo madarakani hivi sasa wakiwa wamesimama au kuketi pamoja. Badala yake tunayo picha hii ambayo tuliitengeneza wenyewe ya Baraza la Mawaziri lililopo madarakani.Kuna fununu kwamba siku si nyingi,Rais Kikwete atafanya mabadiliko katika baraza la mawaziri lililopo.
Sasa badala ya kuweka tu picha na kusema “pichani ni Baraza la Mawaziri na kisha kutoka kushoto kwenda kulia ni yule na yule na yule’,nadhani ni wakati muafaka tukajiuliza,Je unaonaje utendaji wa Mawaziri hawa mpaka hivi sasa?Yupi ambaye unaona anafanya kazi yake ipasavyo na yupi analegalega au kutowajibika kabisa?

Mwaka juzi niliandika kidogo kuhusu umuhimu wa kuandika na kutunza historia zetu hususani mitandaoni katika zama hizi za maendeleo makubwa na ya kasi ya sayansi na tekinolojia.
Nakumbuka niliandika na kuomba wajuzi wa historia ya nchi yetu,kushiriki katika kuandika na kuitunza historia ya Mwanasiasa Mkongwe,Hayati Bibi Titi Mohammed kupitia mradi wa Wikipedia ambao leo hii unasifika na kuaminika kuwa chanzo cha maarifa mbalimbali.Kwa bahati mbaya,mpaka hivi leo ukurasa wa Bibi Titi Mohammed katika Wikipedia bado una mapungufu.Unahitaji kuendelezwa.Ni kweli kwamba hakuna anayejua kwamba Bibi Titi alizaliwa wapi na kwamba hata tarehe yake ya kuzaliwa haijulikani zaidi ya kwamba alizaliwa mwaka 1926?
Pamoja na utata ambao umekuwa ukijitokeza mara kadhaa kuhusu usahihi wa kinachoandikwa katika Wikipedia,hivi leo inasemekana kwamba wanafunzi wengi,hupata maarifa yao kupitia Wikipedia.
Utata unaojitokeza kuhusu usahihi au kinyume chake katika Wikipedia, unatokana na ukweli kwamba Wikipedia inaandikwa na kila mtu.Wewe na mimi.Kila mtu ana uhuru wa kujiunga na Wikipedia na kuchangia.
Hatari ya uhuru huo ni kwamba kuna uwezekano mkubwa wa mtu au watu kuandika historia katika jinsi ambayo itakidhi mahitaji yao na hivyo kuandika habari potofu au za uongo.Hilo linaweza kufanyika kwa bahati mbaya au makusudi.
Kama hunipendi mimi Jeff Msangi,basi unaweza ukaingia katika Wikipedia na kuandika unachokitaka wewe mpaka hapo mwingine anayeijua historia yangu kwa jicho lingine,atakapoingia na kusahihisha.Kama mimi mwenyewe nipo hai pia naweza kuwaandikia Wikipedia na kutoa malalamiko yangu na wao watarekebisha.Kwa kawaida,mtu binafsi haruhusiwi kujiunga na Wikipedia na kuandika habari zake binafsi kwa minajili ya kujitangaza na mambo kama hayo.Historia yako inaandikwa na watu wengine.
Sikumbuki nilikuwa nawaza nini leo nilipoamua kujaribu kutafuta habari zinazomhusu Mwanasiasa mkongwe,Marehemu Oscar Kambona(13th August 1928-July 1997). Historia yake,kwa mujibu wa Wikipedia, imeandikwa vizuri na kwa umakini.Nasema kwa umakini kwa sababu imeandikwa kwa nia ya makusudi ya kuelezea maisha ya mwanasiasa huyo katika miale ya kumtaka msomaji kuelewa vizuri historia yake na kile kilichojiri mpaka akaja kutoelewana na serikali ya awamu ya kwanza na bila shaka Hayati Baba wa Taifa,Julius Kambarage Nyerere mwenyewe. Lakini kila kitu kilichoandikwa pale ni sahihi? Mtiririko ule wa matukio ndivyo ulivyokuwa? Ni kweli kwamba Kambona na Nyerere walishindwa kuelewana katika suala zima la siasa za Ujamaa na Azimio la Arusha peke yake? (Nyerere aliamini katika Ujamaa wakati Kambona aliamini katika Ubepari)

Baraza la Kwanza la Mawaziri baada ya Muungano.Oscar Kambona ni wa tatu kutoka kushoto mstari wa mbele.
Hapo ndipo linapokuja tena suala la sisi sote,hususani wale wasomi wa historia,kuwa mstari wa mbele katika kuchangia katika miradi kama Wikipedia.Nia ni kuhakikisha kwamba historia ya nchi yetu,ya watu wetu,inaandikwa kwa usahihi wa kutosha na unaokubalika. Tusipofanya hivyo,tunahatarisha kuzidi kuupoteza ukweli kuhusu historia.Muda ni jambo la ajabu.Hutufanya kusahau.Vizazi vya baadae vitasoma nini na kujifunza kutoka kwa nani juu ya historia yetu?
Shime.Wewe msomi.Jiunge sasa na Wikipedia.Sahihisha.Andika.Historia yetu,za kwetu,za watu wetu ni muhimu zikaandikwa na watu miongoni mwetu.

Kwa niaba ya Tanzanian Canadian Association (TCA), chama cha jumuiya ya Watanzania tunaoishi Toronto , Ontario , Canada na vitongoji vyake, tunapenda kuchukua fursa hii kwanza kabisa, kutoa rambirambi zetu kwa familia za wananchi waliopoteza wapendwa wao katika ajali ya mabomu yaliyolipuka katika kambi ya jeshi eneo la Gongo La Mboto, Dar-es- Salaam , Tanzania .
Tunawaombea wote waliopoteza maisha yao Mwenyezi Mungu awapumzishe kwa amani; tunawatakia majeruhi waugue pole, wapone haraka ili waweze kuendelea na shughuli zao za kila siku. Vilevile, tunawatakia wote waliopotezana na ndugu zao hususan watoto waliopotezana na wazazi wao waweze kupatikana na kukutana tena.
Tumesikitishwa na taarifa za maafa hayo na kuhuzunishwa kuona kwamba ni mara ya pili tukio kama hili linatokea nchini kwetu. Wengi watakumbuka siku si nyingi janga kama hili lilitokea kule Mbagala. Tunapenda kuuomba uongozi wa jeshi uangalie upya namna silaha kali zinavyohifadhiwa; katika utaratibu wa kuhifadhi mabomu, tunapendekeza yafanyike marejeo na marekebisho yatakayozingatia usalama wa raia.
Katika kuhitimisha, tunalisisitizia Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), lichukue hatua madhubuti na za haraka katika kuhakikisha majanga yanayoweza kuepukika kama haya hayatokei tena.
Mungu Ibariki Tanzania .
Uongozi – Tanzanian Canadian Association (TCA)

This is the official picture of Dr.Mohamed Ali Shein, the recently elected President of Zanzibar.

Rais Jakaya Kikwete akiwa na Majaji wa Mahakama Kuu.Hiyo ilikuwa ni wakati wa shughuli za kumuapisha Jaji Mkuu Mpya,Mohamed Chande Othman,zilizofanyikia katika viwanja vya Ikulu jijini Dar-es-salaam hivi leo.

Jaji Mkuu mpya,Mohamed Chande Othman,akila kiapo mbele ya Rais Jakaya Kikwete na Jaji Mkuu anayestaafu,Jaji Augustino Ramadhani.


sending...

