This episode was aired on EATV on Monday 23rd January 2012.It features one of the few comedian in the land who can actually make me laugh and think at the same time.Steve Nyerere,who recently launched his movie/doc titled Mr.President in which he imitates the life of Tanzania’s current President,Jakaya Mrisho Kikwete, is a comedian with an insight of his own. For example listen to him giving advice on parenting in the 21st century. Then sit down and wait for him to tell you what happens when a rich man passes away! Have you ever thought of it?

Watch this funny episode below and remember that Mkasi TV is exclusively shot at Amaya Beauty Salon & Spa, the leading beautifying centre in Dar-es-salaam.They are located with Air Tanzania Corporation(ATC) compound at the junction of Garden Avenue and Ohio Street in Dar-es-salaam.

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Saleh Ally anajua anachokiongelea.Ni mwandishi wa siku nyingi sana wa habari za Michezo na Burudani.Uzoefu wake ni hazina.Ni lulu.Unapopata kumsikia,unapata maarifa.Ndicho nilichokiona,ndicho nilichokisikia.Nami nikaona usikose.

Mtizame Saleh Ally katika kipindi hiki cha MkasiTv kilichorushwa takribani wiki iliyopita kupitia EATV.Mkasi hurushwa kila Jumatatu saa tatu na nusu usiku.Usiwe unakosa hivi vipindi.Maarifa zaidi katika format rahisi…

Kisha ukitaka nawe kupendeza na kwenda na wakati kama wanavyokwenda nao masupa staa wa nchini,usisite kwenda Amaya Beauty Salon & Spa.

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Kipindi cha Mkasi Tv kinachorushwa na East African Television (EATV) kila siku ya Jumatatu saa tatu na nusu usiku(9:30pm) kinazidi kujipatia umaarufu.Mimi binafsi ni mpenzi na mfuatiliaji mzuri wa kipindi hicho.Huenda ni ule urahisi wake(simplicity) ndio unaonifanya nipende kukitazama.Huenda ni wahojiwa(interviewees ).Huenda ni mandhari(location) kwani kipindi hicho hutokea ndani ya mojawapo ya Salon & Beauty Spa bora kabisa jijini Dar-es-salaam,Amaya Beauty Salon & Spa.Ukitaka kujua mengine kuhusu Amaya,bonyeza hapa. Lakini huenda ni host wa kipindi hicho,Salama Jabir.Napenda simplicity yake,witty na jinsi anavyoendesha mahojiano.Napenda mahojiano kama vile ninavyopenda documentaries. Napenda kujua nisiyoyajua.

Wiki iliyopita Mkasi kilimuangulia model maarufu na wa kimataifa kutoka Tanzania,Flaviana Matata.Endapo hukupata nafasi ya kukiona kipindi kupitia luninga yako pale nyumbani,nafasi ipo wazi kutizama kupitia mtandao.Hili nalo ni mojawapo miongoni mwa niyapendayo kuhusu Mkasi;kwenda na wakati.Kipindi cha television ni vizuri kikipatikana pia mtandaoni.Ikiwezekana nawashauri hawa jamaa wawepo hata katika iTunes ili tuweze kukipata kama Podcast.Kitazame

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

We missed putting these episodes of Mkasi TV which,in my opinion, is one of the best TV shows in the land by now basing on insight interviews which are based on very common atmosphere for us all…the Salon and Spa.

MKASI WITH SHADRACK NSAJIGWA,TAIFA STARS & YOUNG AFRICANS CAPTAIN

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

MKASI WITH MAMA HASHEEM THABEET

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

MKASI WITH JAFFARAI,BONGO HIP HOP ARTIST

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

In case you missed this episode,watch it below.This one features Asha Baraka,a legendary businesswoman who owns a number of entertainment outlets including the famous band,Twanga Pepeta.

Mkasi is exclusively shot at Amaya Beauty Salon & Spa located at the heart of Dar-es-salaam within Air Tanzania Corporation(ATC) compound at the intersection of Garden Avenue and Ohio Street.

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Kama wewe ni mpenzi wa vipindi vya kwenye luninga,ninalo jambo zuri ambalo sina budi kukwambia endapo kwa bahati mbaya tu,yaweza kuwa hujalisikia.Kuna kipindi kipya ambacho hurushwa na EATV kila Jumatatu saa Tatu na Nusu Usiku.Kipindi kinaitwa Mkasi.Kina mahojiano ambayo binafsi yananivutia kwani yanaakisi picha hali ya jinsi ambavyo mazungumzo ya kawaida yanaweza kuibuka mahali pa kujisafi na kujiweka sawa.Mazungumzo hayo yanaweza kukuacha ukiwaza,ukiwazua na kisha ukapata fikra tofauti.Ni ukweli kwamba panapo kupendezeshana au kujiweka sawa,basi watu huongea,hujadili na ndivyo mambo yanavyokwenda. Kimeitwa Mkasi kwa sababu mahali kama Saluni ambapo kwa kiasi kikubwa “Mkasi” ndio hutumika au ndipo zilipoanzia.Siku hizi,of course,vifaa vipo vingi.Lakini Mkasi,ndipo tulipoanzia!

Kipindi hiki cha Mkasi ambacho ni ubunifu wa Salama Jabir na Ambwene Yessayah(AY) hukujia kwako exclusively kupitia EATV huanzia pale Amaya Beauty Salon & Spa ambayo ni Salon & Spa ya kisasa,mpya na ya aina yake jijini Dar-es-salaam.Ipo ndani ya compound ya jengo la Air Tanzania Corporation(ATC) lililopo katika makutano ya Barabara za Ohio na Garden Avenue katikati ya jiji la Dar-es-salaam.Watembelee uone mahali ambapo wajanja wengi wa jiji hili wanapopendezea!

Wiki hii kipindi cha Mkasi kilikuwa na Mchora Katuni maarufu na pia mtangazaji wa Times FM,Masoud Kipanya.Kama hukupata nafasi ya kukitazama,basi usipitwe na uhondo huo.Kitazame hapa chini;

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Ni program ya kijamii ambayo inaenda hewani kupitia kituo cha STAR TV kila JUMAPILI saa 12:30 -1:00 jioni. Ni program mzuri sana ambayo inalenga kuburudisha, kuelimisha, kugusa hisia, pamoja na kugawa “vijisenti.”.Watch the part of the first episode below.

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Hivi msomaji mpendwa umeshwahi kujiuliza ungekuwa unafanya shughuli gani kama sio hiyo unayofanya sasa?Binafsi,ukiweka kando ndoto zangu za kitaaluma,nilikuwa na ndoto nyingine mbili.Moja ni kuwa daktari,ndoto iliyoyeyuka baada ya kupata F kwenye Fizikia na D kwenye Hisabati,japo nilikuwa na A ya Kemia na C ya Bailojia.Nilipofaulu kujiunga na Kidato cha Tano nikaamua kuchukua mchepuo wa Historia,Jiografia na Kiingereza (HGL).

Ndoto ya pili ilikuwa kuwa mtengeneza muziki au prodyuza.Msanii aliyenivutia sana (na anayeendelea kunivutia hadi leo) ni Dr Dre.Bahati mbaya,masuala ya shule yakanielemea zaidi na ndoto hiyo pia ikaenda na maji.Hata hivyo,tangu wakati huo nimekuwa nikiwathamini sana watu wanaofanya kazi kubwa japo haionekani waziwazi na pengine hawafahamiki zaidi ya wanaoonekana.

Chukulia mfano wa prodyuza wa muziki.Wakati takriban dunia nzima inawajua akina Lady Gaga,Beyonce na wengineo,ni watu wangapi wanaowafahamu wanaotunga nyimbo za wasanii hao?Au wataalamu wanao-prodyuzi miziki yao?

Mfano mwingine ni kwenye filamu.Wakati majina yanayovuma ni ya actors na actresses,watengeneza filamu-kwa maana ya waandishi wa script,waongozaji,nk wanabaki kuonekana kwenye shukrani za mwisho wa filamu tu japo wao ndio hasa wanaowawezesha actors na actresses kupata majina na kufanya movies zivunje rekodi za mauzo.

Na unapoangalia runinga,unapata wasaa wa kujiuliza kuhusu watu walio nyuma ya kamera,waandaaji wa kipindi,na wengineo wanaofanya mtangazaji unayemowna kwenye runinga afanye kile unachotarajia kama mtizamaji?

Hizi ndizo sababu zilizopelekea tovuti hii kumsaka Sophia Mwanauta,binti wa Kitanzania anayeishia hapa Uingereza,ambaye ni “moyo” wa utengenezaji wa kipindi maarufu cha Sporah Show,kinachoandaliwa hapa na kurushwa hewani na vituo vya BEN TV ya Uingereza na Star TV ya huko nyumbani.

KWA MAHOJIANO KAMILI BONYEZA HAPA KUELEKEA KWENYE BLOG YA KULIKONI UGHAIBUNI YA EVARIST CHAHALI

Kama utakumbuka wiki kadhaa zilizopita tulikuletea picha kadhaa toka katika location ya making of “Nitarejea” Video by Diamond. The official video is out and here it is for your enjoyment;

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Ndani ya kipindi cha takribani miaka 5 iliyopita, kumekuwa kukianzishwa Reality TV Shows mbalimbali nchini kwetu. Miongoni mwa shows hizo ni pamoja na ile ya Maisha Plus ambayo kwa kipindi kifupi tu tayari ilikuwa imejizolea mashabiki lukuki.Bila shaka mafanikio hayo yalitokana na ubunifu na uhalisia uliombatana na kipindi hicho.

Hata hivyo Maisha Plus ni kama vile imepotea ghafla.Kulikoni?Baada ya kupata maswali kadhaa toka kwa wasomaji mbalimbali na hususani mashabiki wa Maisha Plus,BC ilimtafuta Masoud Kipanya ambaye ndiye mwanzilishi na mratibu mkuu wa Maisha Plus ili kupata ufafanuzi kuhusu hatma ya kipindi hicho.Haya hapa mahojiano mafupi na Masoud Kipanya(KP)

BC: Kwa muda sasa tumekuwa tukipokea maswali kadhaa kuhusu Maisha Plus.Wengi wanataka kujua kulikoni mbona hawasikii chochote na muda wa audition ndio huu?Je mwaka huu kutakuwa na Maisha Plus au ndio basi tena?

KP: Asante kaka kwa kunitafuta ili kujua kinachoendelea. Hii inamaanisha kwamba unatujali na unapenda maendeleo yetu.Ni kweli watu wengi wamekuwa wakiulizia kulikoni. Kuna sababu kadhaa ambazo zimesababisha hali iliyopo ya kuchelewesha mambo kiasi kwamba watu wengine kuona kama vile Maisha Plus imekufa. Ukweli ni kwamba Maisha Plus haijafa.Bado ipo. Kuna mambo kadhaa ambayo yalijitokeza na ndio yanachangia ucheleweshwaji huu. Miongoni mwa mambo hayo kubwa zaidi ni namna season 2 ilivyokwenda.Nitafafanua;

Kwanza kabisa naweza kusema wenzetu wa TBC kwa kiasi fulani walituangusha ingawa nashindwa kuwalaumu moja kwa moja kwa sababu mpaka leo hawajapata nafasi ya kukaa nasi meza moja kujua what happened. Tunafahamu walikuwa bize na uchaguzi na hivi karibuni pamekuwa na mtikisiko wa kuondoka kwa DG wao.

Season 2 ilirushwa vibaya sana in terms of timings. Kuna siku kipindi kilikuwa kinarushwa saa 9 mchana, siku nyingine saa 12 jioni, saa 4 usiku na hata saa 6 usiku.Yaani hakukuwa na ‘consistence’. Na kwa kawaida kipindi cha redio au tv lazima watazamaji wajue time moja, kama itatokea dharura basi mabadiliko ya muda huweza kuvumiliwa mfano nyakati za bunge au kama kuna hotuba ya Rais nk.Hii ilichangia kwa kiasi kikubwa season 2 isitazamwe na watazamaji wengi.

Bahati mbaya kwetu hakukuwa na sababu za msingi zilizowekwa wazi. Najua wasomaji wako watajiuliza kuhusu mkataba wetu na TBC, kwa kuwa tulianza kwa kutumia fedha zetu za mifukoni kutokana na kutokuwa na sponsors, tulikubaliana kwa pamoja, sisi kama waandaaji dmb Co.Ltd na TBC kukibeba kipindi kama wanavyofanya wengine mpaka kitakapochanganya na kuanza kuvuta mashabiki ambao ndio husababisha wadhamini kuingia.

Jukumu lao kwa mujibu wa mkataba wetu lilikuwa kurusha kipindi kwa wakati na sisi tulibeba jukumu la kutengeneza kipindi na gharama zake.

read more

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page