MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

Anaitwa Irene Sporah Njau, ni mtangazaji wa Kipindi cha Sporah Show ambacho kinazidi kujipatia umaarufu na mashabiki.Lakini Sporah ni nani,ametokea wapi,ana malengo gani na ni kwanini anafanya anachokifanya? Ili kupata majibu ya maswali hayo na mengineyo bonyeza hapa kutembelea Spoti Starehe ili kucheki mahojiano kamili.

elizabeth_graf_lg

Yawezekana kabisa ukawa hufuatilii sana show ya Big Brother Africa ambapo watu fulani,wasichana kwa wavulana,huchaguliwa na kwenda kuishi ndani ya jumba moja(Big Brother House) kwa siku zisizopungua 90 huku kila kitu wanachokifanya ndani ya jumba hilo kikifuatiliwa,kurekodiwa na kuonekana kwa kila mwenye nia ya kuona kinachoendelea.

Sababu za kutofuatilia zinaweza kuwa nyingi.Unaweza kuwa huna muda.Unaweza kuwa huoni maana au mantiki ya kuketi mbele ya runinga yako na kutazama watu wengine huku ukitambua kwamba wanachokifanya pale ni kama mchezo wa kuigiza kitu ambacho hakibebi uhalisia.Mimi naamini kwamba wanapoanza ile show huwa wanaigiza.Lakini kadri mtu anavyozidi kukaa katika jumba lile,tabia au hulka yake ya kweli huibuka.Siamini kwamba mtu anaweza kuwa “fake” kwa siku zaidi ya 60!

Sababu za kuangalia pia zipo.Unajifunza mawili matatu.Unajifunza jinsi ya kuishi na watu,kuwasiliana na watu na pengine jinsi ambavyo mtu anaweza kunuia kufikisha ujumbe fulani kwa mwenzake au kwa jamii lakini akashindwa kueleweka au kutimiza lengo lake kutokana tu na uchaguzi mbovu wa maneno.Ukiiangalia show ile,unaweza pia kuona tofauti za kibinadamu miongoni mwa wanaume na wanawake.Sote tuna mahitaji sawa; kupenda,kupendwa,kuthaminiwa,kuheshimiwa nk lakini tuna njia tofauti tofauti za kufikia malengo yetu.

Lakini pia unaweza kujifunza kwamba unapomuona mtu kwa nje,usiwe mwepesi wa kudhani kwamba unamjua na unaelewa kila kitu alichopitia au anachopitia maishani mwake.Hili ndilo nililoliona baada ya kusikiliza ujumbe kutoka kwa binti anayeiwakilisha Tanzania(Elizabeth) katika show hiyo baada ya kutumiwa kipande cha video na msomaji mmoja wa BC.

Kwa wengi,Elizabeth ni binti mrembo mwenye kila nia ya kuendeleza sanaa ya urembo na uanamitindo.Utakumbuka kwamba aliwahi kuwania taji la Miss Tanzania bila mafanikio.Lakini je mambo ni safi au tambarare siku zote kwa Elizabeth? Anapitia au amepitia maswahibu gani maishani mwake? Msikilize Elizabeth katika kipande hiki cha video akiongea na wenzake.Bado huna sababu ya kumpigia kura za kubakia “mjengoni” Elizabeth?

riccoangola

Shindano la tatu la Big Brother Africa limemalizika leo huko Afrika Kusini ambapo kijana kutoka Angola, Ricardo David Ferreira Venancio a.k.a Ricco (21) kama alivyojulikana ndani ya Big Brother House ndio mshindi wa shindano la mwaka huu.

Tofauti na mashindano mengine,shindano la mwaka huu lilibidi liamuliwe kwa mbinde ya kutafuta asilimia ya jumla ya kura zote zilizopigwa mwaka huu baada ya Ricco kufungana na binti kutoka Malawi, Hazel(25)

Hongera kwa Angola kwa kuibuka washindi.


Kama kuna kitu ambacho kilitokea katika upande wa burudani nchini Tanzania hivi karibuni na kuteka hisia za watanzania wengi,bila shaka kitu hicho ni kundi lililokuwa linajulikana kama Ze Comedy.Tunasema lililokuwa linajulikana kama “Ze Comedy” kwa sababu mpaka sasa kuna utata au kesi kuhusiana na haki miliki ya jina hilo!Kesi iko kwa pilato.

Ilifikia kipindi ukimtafuta mtu siku ya Alhamisi jioni(wakati kipindi cha Ze Comedy kipo hewani) usipompata yawezekana kabisa yupo mbele ya luninga yake akiwacheki Ze Comedy huku simu yake akiwa ameiweka katika mtetemko(vibration) katika kumaanisha kwamba “hataki usumbufu”.

Wakati kundi hilo likizidi kujipatia umaarufu mara ghafla zikaja habari kwamba Ze Comedy wanakwenda “mapumzikoni”.Pamoja na kwamba tangazo hilo liliwasikitisha watu,ilieleweka kwamba mapumziko ni jambo muhimu kwa kila binadamu kwa hiyo watu wakaelewa!

Tatizo lilikuja pale mgogoro ulipofumka baina ya Ze Comedy na uongozi wa kituo cha EATV ambacho ndio kilikuwa kinarusha kipindi cha Ze Comedy kila siku ya Alhamisi saa moja jioni.Mapatano ya mezani yakashindikana.Kesi ikaenda mahakamani(bado ipo).Siasa nazo zikaingilia kati.Vigogo wa nchi wakaingilia lakini wapi.

Leo hii watu wengi wanajiuliza,je Ze Comedy watarudi? Na wakirudi watarudi kwa namna gani,kwa kutumia jina gani?Unadhani watakamata tena?Unadhani kilichotokea mpaka hivi sasa kinatoa mafunzo gani kwa vikundi vingine na washika dau wote wa fani ya burudani nchini Tanzania?

Kuna habari ambazo bado hazijaweza kuthibitishwa zinazosema kwamba vijana hao mahiri kwa kuvunja watu mbavu huku wakielimisha jamii wana mpango wa kufanya ziara kabambe nje ya Tanzania.Tunasubiri.

Kama tulivyoahidi,huyu hapa ndio mwakilishi wetu huko South Africa katika shindano la Big Brother Africa III. Jina lake anaitwa Latoya.Ana miaka 21.Ni Katibu Muhtasi.Ukitaka kuwaona washiriki wenzake bonyeza hapa.

Lile shindano maarufu lijulikanalo kama Big Brother Africa linaloendeshwa na kituo maarufu cha televisheni cha Afrika Kusini(M-Net) linaanza tena leo nchini Afrika Kusini huu ukiwa ni msimu wa tatu tangu kuanzishwa kwake.

Jumla ya washiriki 12 wataingia leo kuanzia saa moja jioni tayari kuishi ndani ya jumba la Big Brother kwa siku 91 huku kila wanachokifanya kikirekodiwa kwenye kamera.Mshindi anatarajiwa kupata dola za kimarekani laki moja.

Kama mtakumbuka mshindi wa mwaka shindano lililopita alikuwa Richard Bezuidenhout (pichani) kutoka Tanzania.Majina au sura za washiriki wa mwaka huu bado ni siri ya waandaji na watajulikana pindi shindano litakapokwenda “live”.Pamoja na siri iliyopo kuna habari kwamba safari hii Tanzania inawakilishwa na msichana.Nani atamrithi Richard? Mwakilishi wa Tanzania ni nani?Tutawapasha punde.


Jina lake kamili ni Robert Gathecha Mongi.Wengi hivi leo tunamtambua kama Bobby.Bila shaka kabisa,Bobby ni miongoni mwa wasimamizi mahiri wa shughuli(MC),watangazaji wa radio na televisheni ambao Tanzania ya leo inaweza kujivunia.Awe anasimamia shughuli,radioni au kwenye televisheni ukimsikiliza utagundua jambo moja;anaipenda kazi yake na anaifanya kwa umakini na utulivu wa hali ya juu.Pengine utulivu huo ndio uliomfanya awe ni mtangazaji wa kutegemewa katika vituo mbalimbali vya radio nchini Tanzania na pia msimamizi wa shughuli zenye hadhi za kimataifa.

Pamoja na mafanikio na “soko” ambalo tayari alikuwa ameshajitengenezea,hivi karibuni alifanya uamuzi mgumu wa kuamua kurudi shuleni ili kunoa zaidi kipaji alichonacho.Hivi sasa anasoma katika Chuo Kikuu cha Cape Town nchini Afrika Kusini.Mbali na kuamua kurudi shule,Bobby ndio kwanza alikuwa “amepata jiko” kabla ya kuwa baba mapema baadaye.Mchanganyiko huo wa mambo ndio unaotufanya tuuite uamuzi wake wa kurudi shule kuwa mgumu!How is he handling all these?

Hivi karibuni tulipata nafasi ya kuzungumza naye machache kuhusiana na maisha yake,shule,ndoto zake na mengineyo mengi.Je anasemaje kuhusu Afrika Kusini anaposomea hivi sasa?Anasomea nini?Nini ushauri wake kwa vijana wanaoota kila siku kwenda “bondeni”?Anazungumziaje maendeleo ya muziki na filamu ya Tanzania akilinganisha na Afrika Kusini? Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo; (more…)

Shindano la 57 la kumtafuta Miss Universe 2008 linatarajiwa kufikia tamati Jumapili hii tarehe 13 Julai huko Nha Trang,Khanh Hoa nchini Vietnam katika ukumbi wa Crown Convention Centre.

Kwa mujibu wa taarifa tulizonazo, shindano hilo litaonyesha moja kwa moja au ‘live” katika vituo mbalimbali vya televisheni ulimwenguni huku nchini Tanzania kituo cha TBC 1 kikifanya hivyo pia.

Majaji wa fainali hizo wametajwa kuwa ni Donald Trump Jr(mtoto wa bilionea Donald Trump ambaye pia ndio bosi mkuu wa Miss Universe), Mwanamitindo na mjasiriamali maarufu Roberto Cavalli,muigizaji na mrembo Nadine Velazquez(anaonekana katika show maarufu ya kituo cha televisheni cha NBC iitwayo My Name is Earl), TV Presenter na mshindi wa Miss Universe 2004 Jennifer Hawkins, mtia nakshi maarufu Louis Licari na mpambaji maarufu John Nguyen.Majaji hao watafanya kazi yao katika mavazi ya kuogelea(swimsuit), mavazi ya jioni(evening gowns) na pia ujibuji wa maswali.

MCs wa onyesho hilo watakuwa Jerry Springer na Mel B(kutoka kundi maarufu la zamani,Spice Girls).Burudani inatarajiwa kutolewa na Lady GaGa anayetamba na wimbo wake Just Dance.

BC inamtakia Amanda kila la kheri.Kwa picha zaidi bonyeza “more” hapo chini. (more…)

Amezaliwa mkoani Shinyanga nchini Tanzania tarehe 27 Julai 1983.Ni miongoni mwa waigizaji wa kike nchini Tanzania ambao wanafanya vizuri.Safari yake katika uigizaji ilipata spidi alipojiunga na kundi la sanaa lijulikanalo kama Kaole Sanaa Group.Waigizaji wengi nchini Tanzania wamepitia katika kundi hilo. Jina lake halisi ni Blandina Chagula.Lakini kwa wengi anajulikana kama Johari.

Photo/GP

Bila shaka hujamsahau Nuru Nassoro ambaye kwa wengi hujulikana kama Nora.Kama umemsahau basi kumbukumbu rahisi ni kwamba ni msanii wa maigizo na filamu nchini Tanzania ambaye miaka ya nyuma kidogo aliwahi kujipatia umaarufu na mashabiki kibao.Lakini pia alikuwa kipenzi cha vyombo vya habari.Katika siku za hivi karibuni amekuwa kimya sana kiasi ambacho wengine wamefikia kusema keshastaafu fani.

Hivi majuzi,baada ya kupotea katika macho ya watu kwa muda mrefu, alijitokeza tena wakati wa utoaji wa tuzo za Vinara wikiendi iliyopita pale Diamond Jubilee kama anavyoonekana pichani.Pamoja na kujitokeza,Nora aliwapa watu something to talk about. Bonyeza hapa uone kwanini.

Photo/Ahmad Michuzi.

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page