The video was produced by Louise Kamin and shot by the Danish/Tanzanian cinematographer Talib Rasmussen for Caravan Records. The video was shot in a derelict building belonging to the Egyptian embassy along Kenyatta Drive which has now been torn down. It features some of the musicians who perform with Mzungu Kichaa and the legandary Tanzanian boxer Sheni who met with Mohammad Ali during the “rumble in the jungle” fight in Congo in 1974.
The song is about the process of saying goodbye to a loved one and metaphorically could be interpreted as saying goodbye to life. Mzungu Kichaa sings: ‘We have struggled in this world together and now the time has come to say goodbye. It will make me happy if you smile rather than cry. Who knows if we’ll meet in the heavens? We must respect and help each other here on earth, for we might never return again’.
Twalumba kabotu / Twalumba kabotu mama… baba
Ndugu zangu, nawashukuru sana / Tumepambana katika ulimwengu / Muda umefika wa kuachana / Tuagane kwa furaha sitaki lawama / Ninakokwenda nayo nikuzuri / Majani yanaota na maji yanakwenda / Nitafurahi ukicheka kuliko kusononeka / Kilatukiachana tutaonana tena
Ninaenda zangu, nina kimbia / Ukiniomba kubaki nita anza kulia
Ndugu na jirani, rafiki na mtu flaani / Muko na mimi moyoni / Mola tu ndyio ana jua / Ndiyo maana tusaidiane / Tuheshimiane / Kuna siku tuta achana, peponi je tutaonana? / Ulimwenguni haturudi tena / Tupendane tukiwa hai
One of the things I like doing when I surf the internet is reading the interviews. In most cases,I am an interviewer so when I get a chance to read what other interviewers are asking and what their interviewees are saying, I get over excited. I can, at times,feel my heartbeats going faster. I wanna run,read it faster.Be in the Know! That’s me.
It was,therefore, a great morning for me when I came across an interview featuring Subi a lady who runs www.wavuti.com. I know there are lots of ladies doing a fantastic job of blogging out there. But in my opinion,Subi is a rock. She doesn’t only blogs but also assists a lot of younger bloggers to get where she is or where other bloggers are. She understands what is happening behind the pages full of maneno and photos that a lot of us like to peruse through. I have personally benefited from her “good heart”. When I get stuck with a software issue,I always think of Subi. And she is always there to assist unless she is busy saving lives elsewhere.
Here is the interview she did with Vijana FM(another group of people I admire and appreciate when it comes to dot com stuff and mapinduzi halisi). Well done Subi.
Anaitwa Noni Zondi.Ni msanii,model na muigizaji mzaliwa wa Afrika Kusini mwenye makazi ya kudumu nchini Uingereza.
Noni Zondi

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
MAHUSIANO MABAYA SANA KATI Y A TFF NA AFRICAN LYON FC
Kwa masikitiko makubwa sana, uongozi wa timu ya African Lyon Fc inapenda kuwaeleza watanzania hususani wapenzi wa mpira wa miguu kuwa, katika jitihada zote za timu yetu ya kukuza na kuedeleza soka hapa nchini, Tumekuwa na mahusiani MABAYA SANA na chama cha mpira wa miguu yaani TFF.
Napenda kuweka wazi bila kificho chochote kuwa TFF imekua ikitukandamiza na kutuchafua mbele ya jamii kwa makusudi. Tena ni kana kwamba si mtu mmoja ndani ya TFF bali ni kuwa agenda ya TFF nzima.
Kuanzia kwa Rais wa shirikisho kamati ya mtendaji, kamati ndogondogo na pia sekretarieti cha kusikitisha kama si kufurahisha mpaka kwa walinzi wa milangoni siku za mechi.
Napenda nitoe baadhi ya mifano michache ambayo tunakutana nayo katika jitihada zao za kutuyumbisha pamoja na vilio vyetu vya kila siku.
- RATIBA YA LIGI KUU.
Timu zote ambazo zimekua zikienda kucheza mechi kanda ya ziwa zimekuwa zikicheza mechi zote mbili(yaani kucheza na Toto Fc na Kagera sugar). Kitu ambacho African Lyon Fc chini ya uongozi wetu hatujawahi kukutana nacho.
Nakama hiyo haitoshi mechi yetu ya mwisho wanatupeleka Manungu Turiani kucheza dhidi ya JKT Ruvu na hali sisi na JKT uwanja wetu ni Chamazi alafu wenyeji wa Turiani (mwenye Uwanja wao) Mtibwa wanapelekwa Morogoro kucheza dhidi ya Moro United.
Ni vigezo vipi vilivyowekwa kutupeleka sisi na si Simba wala Yanga. Je hii TFF ni ya Simba na Yanga tu.
- MBWANA SAMATA
Ndugu watanzania, Tumeandika barua zaidi ya 15 kwa sekretarieti,kamati ya haki ya wachezaji, Raisi Tenga. Lakini hakuna yeyote aliyezungumzia jinsi ambavyo Simba imegushi uhamisho wa Mbwana Samatta kutoka African Lyon Fc. Cha kushangaza ndugu Alex Mgongolwa ambaye pamoja na kupelekewa barua yetu TFF ofisini kwake,kaibuka na timu ya Kimbangulila Fc na African Lyon tumeachwa bila hata kusikilizwa.
Napenda kumlaumu kwa nguvu zote ndugu Alex Mgongolwa kwa makusudi yake kabisa tena kwa kukusudia ya kugoma kukaa na sisi na kutisikiliza. Na kwa dharau yake ya kushindwa hata kutujibu japo moja ya barua zetu.
Na kwa kuonyesha chuki za wazi kwetu ni pale ambapo aligoma kukutana na WAFADHILI wetu aliokuja kutoka Marekani na Uarabuni kutaka kujua maswala haya hususani ya MBWANA SAMATTA. Hawa ni watu waliotumia fedha na mda wao kuja nchini kwetu alafu mtu anagoma.
Na si yeye tu aliyegoma hata uongozi wa juu wa TFF uligoma kukutana nao ili hali hawa wote walipata taarifa wiki moja kabla juu ya ujio wa wageni hawa.
Today,one of the prominent blogger,Shamim Mwasha aka Zeze is celebrating her birthday.As a friend and brother,would like to wish her all the best.Keep moving,keep writing,keep inspiring.Happy Birthday.
You can visit her blog via 8020fashions.blogspot.com
Leo ni sikukuu ya kitaifa.Wenzetu wa Visiwani wanakumbuka Siku ya Mapinduzi.Lakini unajua yepi kuhusu mapinduzi hayo?Yalikuwaje?Yaliwezekana vipi? Fungua ukurasa huu na usome kidogo. Pia unaweza kusoma mengi kuhusu historia,mila,tamaduni na desturi za visiwani hapo kwa kubonyeza hapa.
Happy Mapinduzi Day
Msanii mkongwe wa sanaa ya maigizo na filamu,Mzee Fundi Said almaarufu kama Mzee Kipara,hatunaye tena!
Habari za uhakika ambazo BC imezipata,zinapasha kwamba Mzee Kipara amefariki dunia majira ya saa tatu na nusu asubuhi ya leo nyumbani kwake maeneo ya Kigogo jijini Dar-es-salaam.
Msanii huyo maarufu ambaye alitamba tangu enzi za maigizo kupitia radio(Radio Tanzania) mpaka kwenye luninga(hususani ITV) akiwa na kundi la sanaa za uigizaji la Kaole,amekuwa akisumbuliwa na maradhi mbalimbali kwa muda sasa.Ilifikia mpaka wakati pakaitishwa harambee ya kujaribu kunusuru afya yake ambapo wasanii kadhaa walijitokeza katika kusaidia.
Kwa namna yoyote ile,hili ni pigo sio tu kwa familia yake bali kwa tasnia nzima ya filamu na uigizaji nchini Tanzania.Tunaungana na wote katika kuwatakia faraja ndugu,jamaa na marafiki wa Marehemu Mzee Kipara.Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema peponi.Amin
wa Fedha ametaja miradi hiyo katika Ukarabati na Ujenzi wa Miundombinu.
Simama hapo ulipo.Jicheki,jikague juu mpaka chini.Sasa jiulize; katika vitu “ulivyotupia” mwilini,vingapi vinatoka au vimetengenezwa nchini China? Jibu linakushangaza? Well…ukweli huo.Wala usijisikie vibaya.Kitu cha kichina kimetawala sio tu Tanzania bali sehemu nyingi sana duniani.Kinachotofautiana ni kile ambacho mimi nimekuwa nikikiita MADE IN CHINA FOR AFRICA na MADE IN CHINA FOR ELSEWHERE! Kuna tofauti kubwa.
Maudhui hayo ndiyo yaliyomo katika wimbo mpya kutoka kwa msanii Chek D akimshirikisha mwenzake anayeitwa January.Sijapata nafasi ya kuwaona wasanii hawa.Nawatafuta.Kwa kifupi wimbo huu ni kama Comedy fulani.Kama hujacheka siku nyingi,basi wimbo huu unaweza kuwa tiba.Ni kichekesho lakini pia kinachoweza kukufanya ufikiri.Hivi ni kweli tumejiachia hivi kwa Mchina?Tumeangalia mbele kiasi gani au ndio mambo ya kutatua matatizo ya leo pekee?
Anyway,sikiliza kitu cha Kichina-China toka kwa Chek D na January. Wimbo umefanyika pale Combination Sound kwa Man-Water.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.


sending...








