Masaa machache tu yamepita tangu niweke video mbili kuhusu saga linaloendelea baina ya Mr.Sugu na Ruge Mutahaba.Yaelekea haya mambo yanazidi kuwa makubwa kwani muda mfupi uliopita,Sugu amerudi tena kwenye vyombo vya habari kwa nia ya kuweka wazi kile ambacho anakiona kama upotoshaji fulani wa habari na mchakato mzima wa kampeni ya Zinduka.
Ameongea na jamaa wa Global Publishers kama inavyoonekana katika video hiyo hapo chini. Sugu anatoa madai makali.Madai ya Rushwa au hongo!
Kama yupo msanii ambaye kwa sasa,kwa maoni yangu,ndiye balozi mzuri wa Afrika nchini Marekani,basi mwanamuziki huyo ni Akon.Huyu jamaa ni mwafrika kwanza kabla ya mambo mengine.Anaupenda uafrika na hafichi.Kila analolifanya anataka ijulikane wazi kwamba kwao ni Afrika.Mtizame katika wimbo huu wa hivi karibuni unaoitwa Oh Afrika.
Kama wewe ni mtizamaji au mpenzi wa sinema za kutoka nchini Nigeria,bila shaka umewahi kuwaona wachekeshaji wawili wajulikanao kama Aki na Ukwa.Wanasemekana ndio waigizaji wafupi kuliko wote nchini humo.Habari nzuri,kama wewe unapendezwa na vichekesho vya Aki na Ukwa ni kwamba wapo njiani kuja jijini Dar-es-salaam.
Kwa mujibu wa Gazeti la Mwanaspoti,wachekeshaji hao wanatarajiwa kufanya vitu vyao katika tamasha la watoto yatima, na wale wanaoishi katika mazingira magumu Februari 14 mwaka huu. Tamasha hilo linatarajiwa kufanyika siku ya wapendanao(Valentine’s Day) katika viwanja vya TTCL, Kijitonyama jijini Dar es salaam.
Aki na Ukwa watakuwa nchini kwa lengo wa kucheza na kufurahi na watoto mbalimbali wahishio kwenye mazingira magumu.
Watasindikizwa na wasanii wengine wa ndani wanaotarajiwa kutumbuiza katika tamasha hilo ni pamoja na Ze Comedy, Q-Chief, Mr.Nice, Rose Mhando na Mrisho Mpoto. Kwa habari zaidi bonyeza hapa.

Mabingwa wa Ligi ya mpira wa kikapu nchini Marekani(mara nyingi hujiita World Champions) kwa mwaka wa 2009,L.A.Lakers,jana walitembelea White House.
Pichani ni manahodha wa L.A.Lakers,Kobe Bryant na Derick Fisher(mbele karibu na Rais Barack Obama) wakimkabidhi jezi na mpira. Rais Obama sio tu ni mpenzi mkubwa wa mpira wa kikapu bali ni mchezaji mzuri wa mchezo huo.Are you an L.A.Lakers fan?

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda ana kama Sh25 milioni kwenye akaunti yake, nyumba tatu za kawaida zilizo Dar, Mpanda na Dodoma na gari alilolinunua kwa mkopo.
Ili kujua zaidi kuhusu alichonacho” Mtoto wa Mkulima” mtembelee Yahya Charahani kwa kubonyeza hapa

Mr.Blue.Ukitaka kusikiliza wimbo wake wa hivi karibuni unaoitwa Tuko Pamoja nenda pale GetMziki
Photo:GetMziki

Tangu apatwe na msururu wa mikasa,Tiger Woods,hajaonekana.Hata marafiki zake kama vile Charles Barkley na Michael Jordan(NBA super stars),wanasema hawajamuona wala kumsikia.Vyombo mbalimbali vya habari za celebrities vimekuwa vikifuatilia uvumi kwamba yupo Florida na bado anajirusha na Rachel (yule mvunja ndoa wa kwanza).Mara ikasemekana ameonekana hotelini New York ambapo aliagiza mvinyo na kujivinjari na vimwana wengine katika hotel.
Lakini juzi,kuna mtu wa karibu yake amejitokeza na kusema Tiger alimwambia kwamba anaenda kwenye Africa Safari. Kwa mujibu wa tovuti ya TMZ, mtoa habari huyo alisema Tiger alikuwa na uhakika kabisa na alichokuwa akikisema.
Sasa mojawapo ya nchi ambazo zinasifika ulimwenguni kwa African Safari ni yetu ya Tanzania.Nchi nyingine ni kama vile Kenya,South Africa,Botswana nk.Hapo ndipo swali linapokuja,je Tiger Woods yupo Tanzania akivuta pumzi na kupumzika mpaka hapo mwakani atakaporejea kwenye proffessional golf?
Hivi sasa mke wake tayari ameshampata wanasheria wa masuala ya talaka(divorce attorneys) ili kuangalia uwezekano wa kupatiwa chake au kwa kizungu structured settlement.
Pichani ni Tiger Woods kama atakavyoonekana katika ukurasa wa mbele wa jarida la VanityFair la mwezi ujao.

Pichani ni Rais wa Afrika Kusini,Jacob Zuma,akicheza ngoma ya asili ya ki-Zulu na mkewe mpya,Thobeka Madiba,katika harusi yao iliyofungwa huko kijijini kwao katika jimbo la KwaZulu.
Kuna mtu kauliza,mbona kuna watanzania wanamshambulia Rais Zuma kwa kuwa na wake watatu?Mbona Rais wetu mstaafu alikuwa na wake wawili?
Picha ya AFP
Leo tukiwa katika siku ya mwisho ya mwaka 2009 na tukijiandaa kuingia mwaka mpya wa 2010, tumepatwa na habari za msiba wa Kiongozi mwanzilishi wa Taifa letu Simba wa Vita Mzee Rashidi Mfaume Kawawa. Kwa Mtanzania yeyote kifo hiki ni pigo kubwa sana, lakini pia ni fursa ya kukumbuka vyema historia ya Tanganyika na Tanzania. Ni fursa ya kuona Watanzania waliojitoa kuona kuwa kunakuwa na Taifa kutoka miongoni mwa nchi iliyokuwa ni mkusanyo tu wa makabila zaidi ya 120. Watu waliojitoa bila kuwa na uzoefu wowote wa si tu kuongoza serikali bali muhimu zaidi uzoefu wa kukusanya makabila, dini na wasio na dini na kuunda Taifa moja imara na la kujivunia linaloitwa Tanzania. Mzee Rashidi Mfaume Kawawa ni mmoja wa watu hawa waliorithi kutoka kwa mkoloni mwingireza nchi iliyokuwa na wakazi takribani milioni 8, isiyo na chuo kikuu hata kimoja, yenye madaktari wawili tu na isiyo na mfumo kabisa. Uhai wa mzee Kawawa, kuwepo kwake na kupumua kulitupa ahueni kuwa tunapo pa kukimbilia na kujifunza kama lolote lingetokea.
Mzee Kawawa ni mfano wa kuigwa kuhusu maana halisi ya utumishi wa Umma. Alikuwa jemedari wa kutegemewa katika utekelezaji wa Dira na ajenda za kujenga Taifa bila kujali maumivu yake kisiasa. Sisi vijana tuliozaliwa miaka ya sabini mwishoni mpaka themanini hatukuona kwa jicho la kuelewa kipindi kigumu cha ujenzi wa Taifa na ujenzi wa Ujamaa nchini. Hata hivyo tulikuwa tukisikia wakubwa wakizungumza na kummlaumu sana Mzee Kawawa kutokana na utekelezaji wa sera mbalimbali kana kwamba zilikuwa ni zake na sio maamuzi ya vikao vya TANU na Serikali iliyokuwa inaongozwa na TANU. Tukiwa masomoni tumejifunza kuwa (more…)

Unaweza kutoa caption(maelezo mafupi) ya picha hii?

