Yanga wakifurahia mojawapo ya magoli kutoka katika mechi hiyo. Picha kwa hisani ya Bin Zubeiry Blog
Timu ya soka ya Yanga, jioni hii imewadhihirishia mashabiki wao na wapenzi wa soka barani Afrika kwamba msimu huu ulikuwa wao baada ya kuwachapa wapinzani wao wa jadi,Simba kwa jumla ya magoli 2-0 katika mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara mchezo ambao ulionyeshwa kote barani Afrika kupitia SuperSport East 9 ndani ya DStv.
Mashabiki wa soka nchini Tanzania na barani Afrika waliweza kuona mpambano huu wa watani wa jadi Live kupitia kwenye luninga zao kwenye SuperSport 9 East ambao walirusha matangazo hayo moja kwa moja kutokea Uwanja wa Taifa.
Katika mchezo huo magoli ya Yanga yalifungwa na Didier Kavumbagu kunako dakika ya 5 ya kipindi cha kwanza na Hamis “Diego” Kiiza kunako dakika ya 63 ya kipindi cha pili.
Kwa matokeo hayo, Yanga inamaliza msimu wa Ligi Kuu ikiwa na pointi 60, ikifuatiwa na Azam FC yenye 52 na Simba 45.Hii ni mara ya 24 kwa Yanga kutwaa taji la Ubingwa wa Soka Tanzania Bara. Hongera kwa Yanga!
Jumapili hii Mei 19 kuanzia saa Kumi na Moja jioni hadi Saa Mbili usiku karibu uburudike na muziki laini wa Jazz ukiletwa kwako na Wakwetu Jazz Vibes pamoja na mpiga gitaa nguli, Jessie. Njoo ujumuike na marafiki pamoja na jamaa wengine Velisa’s Beach. Usisahau kuwaambia na wenzako.

Sijui…lakini nadhani sijawahi kumsikia Diamond akiongelea mahusiano yake na wanawake mbalimbali ukiwemo uhusiano wake na Wema Sepetu ambao mara kwa mara umekuwa lulu ya magazeti ya udaku, mitandao ya kijamii nk.
Hivi karibuni alipofanya mahojiano na Sporah katika The Sporah Show, Diamond alikuwa tayari kuweka bayana mambo kibao. Ni kwanini alimrekodi Wema Sepetu hivi karibuni? Ni kwanini amekuwa hatulii kwa mwanamke mmoja? Anapenda mwanamke wa namna gani? Ana mipango gani na mwanamke aliyenaye hivi sasa ambaye ana ujauzito wake? Tizama hapa chini interview yake;
Umewahi kujiuliza ni msanii gani wa kike wa Bongo Movies ambaye analipwa mkwanja mrefu zaidi endapo mtu anamuhitaji ashiriki kwenye filamu yake?
Mtandao wa FilmCentral unaodili zaidi na masuala ya movies nchini Tanzania, unasema kwamba Wema Sepetu ndiye anayelipwa zaidi kwani ukitaka kumtumia kwenye movie yako ni lazima utoe Milioni 10.
Unaweza kusoma habari hiyo zaidi kwa kubonyeza hapa.
Mabingwa wa Ligi Kuu nchini Uingereza, Premier League ,Manchester United, wametangaza kwamba, Sir Alex Ferguson atastaafu kama meneja wa klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu.
Sir Alex anatajwa kuwa ndiye meneja mwenye mafanikio makubwa katika historia ya soka la Uingereza.
Tangu alipojiunga na klabu hiyo mnamo mwaka 1986, ameshinda mataji mawili ya Klabu Bingwa Barani Ulaya, mataji kumi na tatu ya Ligi Kuu na Kombe la FA mara tano.
Katika taarifa yake, Sir Alex amesema ni muda muafaka kwake kustaafu wakati klabu ikiwa imejizatiti katika nafasi nzuri. Atabakia Manchester United kama mmoja wa wakurugenzi na balozi.
Chanzo: BBC Swahili.

Baada ya hivi karibuni kuamua kuhamishia makazi yake kimaisha na kimuziki nchini Kenya, yaelekea ile tungo ya Nabii hakubaliki nyumbani kwao inazidi kushika kasi. Kwanza ilikuwa ni kama vile kuanza upya muziki baada ya kuwa signed na record label ya nchini humo Grandpa Records na sasa ni upande wa mapenzi.
Kwa mujibu wa mtandao wa Daily Post wa nchini humo, Mr.Nice inasemekana hivi sasa “anabanjuka” na mrembo anayeshikilia taji la Miss Kenya 2012, Shamim Nabil. Mtandao huo unaripoti kwamba wawili hao wamekuwa wakionekana sehemu mbalimbali na wakiwa na ishara zote za mapenzi.
Mtandao huo unazidi kusema kwamba Mr.Nice ameahidi kumuoa binti huyo kwani wasichana wa Tanzania wamemuangusha na hivyo anaona ni bora akawaletea wifi kutoka huko.
Picha: Daily Post.
Here is a story of a young man who recently made President Uhuru of Kenya laugh. As it turned out, it was his way to even greater things. Check these two videos
Kwa muda sasa pamekuwepo na malumbano(japo ya upande mmoja) kati ya Mwanamuziki Lady JayDee ambaye anajiandaa kuachia album yake ya 6 mwishoni mwa mwezi huu na Wakurugenzi wa Kituo Cha Radio na Televisheni cha Clouds FM na Clouds TV, Ruge Mutahaba na Joseph Kusaga na pia baadhi ya watangazaji wa kituo hicho.
Baada ya kuwa kimya kwa muda, na Ruge Mutahaba naye ameamua kujibu tuhuma au shutuma. Sikiliza Clip hapo chini kutoka kwenye kipindi cha Power Breakfast. Then Be The Judge.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.




sending...



















