Wasanii mbalimbali kutoka Nigeria, Kenya na Afrika Kusini wanatarajiwa kupamba shughuli ya kuanza kwa msimu mpya wa show kabambe ya Big Brother Africa siku ya Jumapili tarehe 26 May.Show ya msimu huu imepewa jina la The Chase. Jumla ya washiriki 28 ambao wamechaguliwa kushiriki show ya mwaka huu watatambulishwa rasmi siku hiyo katika tukio ambalo linatarajiwa kuonyeshwa “Live” katika nchi zizizopungua 50.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari, tukio hilo litaanza kuonyeshwa saa moja jioni kwa saa za Afrika ya Kati (19:00 CAT) katika AfricaMagic, AfricaMagic Entertainment, AfricaMagic World na pia kwenye channel 197 na 198 katika DStv.
Msanii kutoka nchini Kenya,STL anayetamba na vibao vyake kama vile “Take My Time” , “Hula Hoop“, “Bad as I Wanna Be“, mshindi wa tuzo za Kisima, Clops na Jeermaan ameahidi kuzikonga vilivyo nyoyo za mashabiki wa muziki na hususani mashabiki wa Big Brother Africa.
Taarifa hiyo inazidi kupasha kwamba kutoka nchini Nigeria, wasanii Don Jazzy, D’ Prince n’ Wande Coal wanatarajiwa kuwakamata vilivyo mashabiki. Don Jazzy, mshindi wa tuzo mbalimbali kama prodyuza, mwimbaji na mwandishi na mwanamuziki atakuwa bega kwa bega D’ Prince na Wande Coal wakitumbuiza na vibao vyao kama vile “I like What I See”, “Bumper 2 Bumper” na “Who Born the Maga”.
Kisha kundi maarufu la muziki wa Afro Pop kutoka Afrika Kusini la Mafikizolo linatarajiwa kuwa kivutio cha kipekee wakati za uzinduzi huo. Kundi hilo ambalo mpaka sasa limeshaweka kibindoni tuzo mbalimbali linatarajiwa kuteka mashabiki kwa nyimbo zao kama vile ”Sibongile”, “Ndihamba Nawe”, “Nisixoshelani” na “Khona”.
Upo msemo wa Kiswahili unaosema “Mafahali wawili wapiganapo,ziumiazo ni nyasi”. Kama kuna ukweli wowote kwenye msemo huo, basi ni dhahiri kwamba wanapombana Yanga na Simba, nyasi lazima ziumie kwani wakongwe hao wa soka nchini Tanzania naweza kuwafananisha na mafahali.
Jumamosi hii, tarehe 18 Mei,2013,Yanga (watoto wa Jangwani) ikiwa tayari imeshanyakua ubingwa wa msimu huu wa Ligi Kuu Tanzania inayodhaminiwa na Vodacom 2012/2013, inateremka dimbani kumenyana na watani wao wa jadi Simba (watoto wa Msimbazi) pale katika Uwanja wa Taifa jijini Dar-es-salaam.
Yapo mambo kadhaa yanayolifanya pambano la Jumamosi kuwa gumzo. Kwanza Yanga tayari ni mabingwa na hivyo kufungwa na Simba katika mpambano huu kitakuwa ni kitu ambacho kimeingiza “shombo” kwenye raha ya ubingwa. Lakini pia Yanga bado wana kisasi moyoni. Utakumbuka Yanga katika siku za hivi karibuni walifungwa 5-0 na Simba. Naam, bado wana donge.
Lingine kubwa linaloufanya mpambano huu kuwa tofauti ni kwamba huko mitaani na hata majumbani,badala ya kusikiliza matangazo ya mpambano huu kupitia radioni (kama tulivyokuwa tukifanya enzi zile za watangazaji kama vile Ahmed Jongo,Charles Hillary nk) safari hii Ulimwengu wa Mabingwa (SuperSport) ndani ya DStv wataonyesha mpambano huo Live kupitia channel ya SuperSport 9 East (Namba 219) kuanzia Saa 10 Jioni.
Kazi kwako mpenzi wa soka. Kazi kwako shabiki wa Yanga au Simba. Una kila sababu ya kulipia akaunti yako ya DStv na kuhakikisha kwamba unaona SuperSport 9 East (channel 219) ili ushuhudie “Live” kila kitakachokuwa kinaendelea kutoka Uwanja wa Taifa. Je ni Yanga au Simba?
Meneja Uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo na Meneja Masoko wa Kampuni hiyo Furaha Samalu katika hatua za mwisho za maandalizi kabla ya kuwasili kwa mgeni rasmi.
Meneja Mkuu wa Multichoice Tanzania Bw. Peter Fauel akisalimiana na Mgeni rasmi Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa mara baada ya kuwasili kuzindua tawi jipya la ofisi za DStv Tanzania lilolopo Kariakoo barabara ya Msimbazi karibu na Diamond Trust Bank jijini Dar. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Multichoice Tanzania Balozi Ami Mpungwe.
Mgeni rasmi Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akisalimiana na Meneja Uhusiano wa MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi mara baada ya kuwasili. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Multichoice Tanzania Balozi Ami Mpungwe.
Meneja Uhusiano wa MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi akiwakaribisha wageni waalikwa na wakazi wa jijini Dar kwenye hafla fupi ya uzinduzi wa tawi jipya la Ofisi za DStv zilizopo Karikakoo barabara ya Msimbazi karibu kabisa na Diamond Trust Bank ambapo amesema Mutlichoice Tanzania inawajali wateja wake ndio maana imeamua kusogeza huduma hizo karibu na wateja wake na kuwataka Watanzania kujipatia king’amuzi cha DStv pamoja na huduma ya ufungaji kwa bei poa ya Tshs 149,000 tu ofa hii ni kwa kipindi cha wiki moja kuanzia tarehe 13th May mpaka 18th May, 2013.
Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Multichoice Tanzania Balozi Ami Mpungwe akizungumza machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kuzindua tawi hilo katika sherehe zilizofanyika jana jijini Dar.
Mgeni rasmi Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akitoa nasaha zake wakati wa uzinduzi wa tawi jipya la Ofisi za DStv zilizopo Kariakoo barabara ya Msimbazi karibu na Diamond Trust Bank jijini Dar.
Mstahiki Meya Jerry Silaa amewapongeza Multichoice Tanzania kwa kuwa wakongwe wa Digitali Tanzania na kuwataka kuendelea kutoa huduma bora zenye viwango ili kuendelea kuwa vinara wa kutoa huduma ya Digitali Tanzania na pamoja na hayo amefurahishwa kusogezwa karibu kwa huduma DStv katikati kabisa ya jiji zitakazowasaidia wakazi Manispaa ya Ilala.
Meneja Uhusiano wa MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi akiwakaribisha wageni wanahabari katika hafla mchapalo ya kusheherekea Africa Day na Dstv ambapo amesema DStv inatoa nafasi kwa wateja wake kuwa na fursa ya kuchagua vifurushi mbalimbali kulingana na uwezo wa mteja ambacho cha uwezo wa chini kabisa ni Access chenye zaidi ya channeli 40 gharama yake ni nafuu sana ambapo mteja atalipia shilingi 16,500 kwa mwezi. (Picha na Zainul Mzige wa dewjiblog).
Meneja wa Fedha wa kampuni ya Multichoice Tanzania, Bw. Francis Senguji akizungumzia malengo ya DStv Tanzania ambapo amesema wao kama waendeshaji wa biashara nyingine barani Afrika wanaojali na kuthamini maendeleo ya jamii wameona ni wajibu kusaidia jamii ili kuweza kuendeleza maendeleo ya kijamii nchini Tanzania.
Kwa kuendeleza hilo Multichoice ina mfumo wa kutoa elimu mashuleni ( Multichoice Resource Centre) hivyo watamumia jukwaa la Teknolojia kama darasa kwa njia mbalimbali kuwapa jamii nafasi ya kuendeleza vipaji na ujuzi.
Mfumo huo kutoa rasilimali kwenye shule kama vile ving’amuzi vya Satellite, VCRs/DVD na kifurushi cha elimu cha Dstv. Mpaka sasa Multichoice imeanzisha vituo vya rasilimali jamii katika shule 82 nchi nzima kwenye mikoa ya Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Iringa, Kagera, Mbeya, Pwani na Tanga.
Meneja Uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo (katikati) akifafanua jambo wakati wa hafla mchapalo katika kusheherekea usiku wa Africa Day na DStv. Kulia ni Meneja Masoko wa Kampuni hiyo Furaha Samalu na kushoto ni Meneja Uhusiano wa Kampuni hiyo Barbara Kambogi.
Waalikwa katika hafla mchapalo ya kusheherekea usiku wa Africa Day na DStv katika Hoteli ya New Africa ya jijini Dar usiku wa kuamkia leo.
Kutoka kushoto ni Meneja Masoko wa Multichoice Tanzania Furaha Samalu, Blogger John Bukuku wa Fullshangwe Blog, Meneja Uendeshaji wa kampuni hiyo Ronald Shelukindo, Mdau wa DStv na Meneja wa Fedha katika kampuni hiyo Bw. Francis Senguji wakipozi kwa picha.
Meneja Uhusiano wa MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi (kulia) akifurahi jambo Wanahabari Sidi Mgumia (katikati) na Mama Mhina.
Ronald Shelukindo na Mdau LEMUTUZ wa Blog ya jamii.

KWA HABARI,PICHA, MATOKEO NK JIUNGE NA UKURASA MAALUMU WA DStv TANZANIA NDANI YA FACEBOOK. BONYEZA JUU YA PICHA HAPO JUU.

Msanii nguli wa muziki wa kizazi kipya Juma Nature akiwapagawisha mashabiki waliofurika katika ufukwe wa Coco beach wakati wa Tamasha la Cheka Nao lilioandaliwa na Vodacom Tanzania kwa ajili ya kusherehekea sikukuu ya Wafanyakazi mei mosi juzi jijini Dar es Salaam.
Mwimbaji wa bendi ya muziki wa dansi ya Msondo ngoma baba ya muziki Romarii Mng’anda akiwaongoza waimbaji wenzake wakati wa tamasha la ChekaNao liliandaliwa na Vodacom Tanzania ikiwa ni mahususi kwa ajili ya kusherehekea sikukuu ya wafanyakazi Mei mosi hapo juzi na kufanyika katika ufukwe wa Coco Beach jijini Dar es Salaam.
Wasanii wa Kikundi cha wakali dansi wakionyesha ukali wao wakati wa onyesho la Cheka Nao liliandaliwa na Vodacom Tanzania katika ufukwe wa Coco Beach jijini Dar es Salaam,Ikiwa ni sehemu ya Kusherehekea sikukuu ya Mei mosi hapo juzi
Msanii anaechipukia wa Kizazi kipya Dogo Lila toka kundi la TMK Wanaume Halisi akionyesha umahiri wake wakati alipokuwa akiimba kwenye Tamasha la Cheka Nao lililoandaliwa na Vodacom Tanzania katika ufukwe wa Coco Beach jijjni Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya sikukuu ya wafanyakazi Mei mosi hapo juzi.
Mzunguko wa pili wa miamba minne iliyobakia kwenye Ligi ya Mabingwa wa Ulaya (UEFA Champions League) unaanza leo. Je, Timu za Spain (Real Madrid na Barcelona) zitaweza kurudisha vipigo zilizopata kutoka kwa timu za Ujerumani (Bayern Munich na Borussia Dortmund). Tizama kupitia DStv Pekee!

Pichani kutoka kushoto ni Barbara Kabogi, Meneja Mahusiano wa Kampuni ya MultiChoice Tanzania, Furaha Samalu, Meneja Masoko wa Kampuni ya MultiChoice Tanzania na mshindi wa DStv Rewards aliyeibuka na Tshs,5,000,000 (Milioni 5), Adelaide Leshabary.
Kwa mara nyingine tena, DStv Rewards imepata mshindi. Aliyeibuka mshindi ni Adelaide Leshabary ambaye, kama wengine 9 waliopita, ameibuka na kitita cha Tshs. 5,000,000.
DStv Rewards ambao ulikuwa mpango maalumu wa kampuni ya MultiChoice Tanzania kuwashukuru na kuonyesha ishara ya kuwathamini wateja wake ulianza tarehe 5 February mpaka tarehe 10 April 2013. Kila wiki mteja mmoja aliibuka mshindi na kujizolea Tshs 5,000,000.

Adelaide Leshabary akiwa na tabasamu kali la ushindi.
Akiongea wakati wa shughuli ya kumkabidhi Adelaide Leshabary kitita chake, Meneja Masoko wa MultiChoice Tanzania,Furaha Samalu, alisema anapenda kuwakumbusha wateja wa DStv kwamba ile ofa ya punguzo la asilimia 10% kwa wateja wanaolipia account zao kabla ya kukatika inaendelea na ni kwa wateja wanolipia vifurushi vyote DStv Access, DStv Compact Dstv Compact family, DStv Compact Plus, DStv premium.
Pia MultiChoice Tanzania inapenda kuwakumbusha wateja wote kwamba wanaweza kulipia huduma za DStv kupitia Mpesa, TigoPesa, Airtel Money, NMB Mobile, Selcom, Maxmalipo na mawakala wa DStv waliopo nchi nzima. Kabla hujalipa hakikisha kwamba Dikoda yako imewashwa au kwa maneno mengine ipo ON.
Endapo itatokea kwamba hata baada ya kulipa huduma yako haijarejea,tuma SMS kwenda namba 15727 yenye ujumbe Reset na kasha weka namba ya kadi yako.Huduma itarejeshwa mara moja.
Kwa maelezo zaidi tembelea www.dstv.com na uchague Tanzania.




sending...





































