MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

Josefina Nunez, Miss British Virgin Islands 2010; Qory Sandioriva, Miss Indonesia 2010; and Hellen Dausen, Miss Tanzania 2010, pose in their Dar Be Dar swimsuits during the registration and fitting process in preparation for the Miss Universe 2010 Competition at Mandalay Bay Hotel and Casino in Las Vegas, Nevada on Sunday, August 8, 2010. The Miss Universe 2010 competition that will air live on the NBC Television Network at 9 PM ET, August 23, 2010

Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Prof.Jay,bado anaendelea na tour yake ndani ya USA.Hapo jana ilikuwa zamu ya watu wa Washington,DC kupata burudani kutoka kwa msanii huyo.Mambo yote yalifanyikia ndani ya sehemu maarufu ijulikanayo kama Zanzibar.

Wikiendi ijayo ni zamu ya watu wa Boston,Massachusetts.

Prof.Jay jukwaani.

An admiration look.Can you spot it?

People showed up and had a good time.

Unapoongelea wanamuziki wa muziki wa kizazi kipya ambao miziki yao na mashairi yao yametoa mchango mkubwa katika kuufanya muziki huo ukubalike na kupewa heshima na nafasi yake katika jamii,bila shaka huwezi kuthubutu kumweka pembeni Joseph Haule au kama anavyojulikana miongoni mwa washabiki na wadau wa muziki; Proffessor Jay,MC Shupavu,The Heavy Weight MC,Jay wa Mtulinga,Mti Mkavu,Jiizeh nk.

Hivi sasa Prof.Jay yupo nchini Marekani akiendelea na tour yake ndani ya taifa hilo ambalo hivi sasa linaongozwa na Barack Obama,Rais wa kwanza mweusi. BC ilipata nafasi ya kufanya naye mahojiano kuhusiana na ziara hiyo. Je unataka kujua atatua na kufanya shows katika miji na majimbo gani? Anasemaje kuhusu ambacho ameweza kukiona na kujifunza nchini humo mpaka hivi sasa? Kwa majibu ya maswali hayo na mengine,fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo;

BC: Prof,asante kwa nafasi hii ya mahojiano mafupi.Mambo yanakwendaje?

PROF.JAY: Safi vipi mtu wangu?Na mimi nashukuru kwa kunipa nafasi hii adimu.

BC: Ni muda sasa umekuwa nchini Marekani kwa ajili ya American Tour yako kiasi kwamba mashabiki wako ambao hawajui uko wapi wamekuwa wakijiuliza maswali yasiyo na majibu ya haraka.Kupitia hapa BC unaweza kuwaeleza kwa sasa hapo Marekani makazi yako ni katika State au Jimbo gani?

PROF.JAY: Asante na naomba niseme samahani kwa wale ambao wamekuwa wakijiuliza kwamba nipo wapi na mambo kama hayo.Kwa sasa hapa nchini Marekani nipo Massachussets nikiwa nimeweka kambi na DJ wangu anayekwenda kwa jina la RICHMAKA.Na sababu ya kuweka kambi hapa ni ili kupata muda wa kutosha wa kufanya mazoezi kwa pamoja kama team ili shows ninazofanya ziwe katika kiwango cha hali ya juu na mashabiki wangu wapate thamani halisi ya pesa zao watakazotoa ili kuja kwenye shows.

BC: Ni kampuni gani inakusimamia katika hii tour yako hapo nchini Marekani?

PROF.JAY: Kampuni inayonisimamia inaitwa NGOME ENTERTAINMENT.Makao yake makuu yapo Dallas,Texas.Kampuni hii ipo chini ya CEO wake,Kitova Mungai.

BC: Ni miji gani ambako unatarajia kuwa na shows?

PROF JAY: Mpaka hivi sasa nimeshapiga show moja ambayo ilifanyikia pale Houston,Texas tarehe 4 Julai(siku ya kusheherekea Uhuru hapa nchini Marekani) Ratiba ya shows zinazofuatia ni kama ifuatavyo:

  • Tarehe 31/8/2010 Washington,D.C
  • Tarehe 7/8/2010 Boston,Massachusetts.
  • Tarehe 13/8/2010 Dallas,Texas.
  • Tarehe 19/8/2010 Kansas City,Missouri.
  • Tarehe 20/8/2010 Witchita,Kansas.
  • Tarehe 11/9/2010 Atlanta,Georgia.

Mpaka hivi sasa ratiba ndio hiyo. Lakini kuna shows zingine nyingi ambazo zinaweza kutokea kwa sababu Promoters kadhaa wameonyesha nia na kufanya majadiliano ya awali ingawa hatuja-confirm firm tarehe kamili za kufanya kazi. Pia naomba niweke wazi kwamba milango ipo wazi kwa promoters wengine ambao wanataka kubook shows.Wenye nia hiyo wanaweza kuwasiliana na Kitova kwa kutumia nambari ya simu +1 214 455 5082 au DJ Rich Maka kwa nambari +1 413 262 0400.Karibuni sana.

BC: Unawaambia nini mashabiki wako katika miji hiyo?Watarajie nini kutoka kwako?

PROF.JAY: Kama nilivyogusia hapo juu,mashabiki wategemee shows za kiwango cha juu kabisa ambayo hawajawahi kuiona kutoka kwa msanii yeyote kutoka kwenye ukanda wa Afrika Mashariki,kati na Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Ninachowaomba wajitokeze kwa wingi ili wasije wakayakosa yale niliyowaandalia.Pia nawaomba wapatapo habari hii wawaambie na wengine.

BC: Waswahili wanasema kutembea kwingi ni kuona mengi pia.Mpaka hivi sasa unaweza kusema umejifunza nini kutokana na ambacho umekiona nchini Marekani iwe ni kwa upande wa sanaa ya muziki au jamii kwa ujumla?

PROF.JAY: Kwanza kabisa nimejifunza professionalism. Huku watu wanaheshimu sana kazi zao. Muda wa kazi ni muda wa kazi. Pia muziki wa huku upo katika kiwango cha juu. Bila shaka na sisi tunahitaji marekebisho mengi sana ili nasi tuboreshe miziki yetu na kazi zetu za sanaa zifikie angalau robo tatu ya kiwango ambacho wenzetu wameshafikia.Nasema hivyo kwa sababu huku muziki ni kazi na ni ajira kubwa sana kwa vijana na hata wasio vijana.Inaheshimika kama kazi nyingine zingine zozote.

Kila anapofanya show,umati kumbi na viwanja huwa “vinatapika”.Hapo ilikuwa ndani ya CCM Kirumba-Mwanza.Can you do a count from this photo?

BC: Baada ya Tour yako nchini Marekani unatarajia kuelekea katika nchi nyingine kuendelea na tour au utarudi kwanza nyumbani kupumzika kidogo?

PROF.JAY: Baada ya kukamilisha hii tour,nitarudi nyumbani kwa mapumziko mafupi kisha nitaelekea Ulaya kwa tour nyingine.Mpaka sasa nimeshapata mwaliko kutoka nchi za Scandinavia(Sweden,Norway,Denmark na Finland).Pia nimepata mwaliko wa kwenda kutumbuiza nchini Uingereza. Nitakaporudi nyumbani ndio nitajua wapi pa kuanzia.Mashabiki na wadau watajulishwa kuhusu tour hizo kupitia vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo BongoCelebrity.

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

BC: Mbali na hiyo tour kuna shughuli nyingine unafanya huko Marekani?

PROF.JAY: Ni kweli kabisa.Mbali na tour pia narekodi miziki.Tumeshaongea na kampuni moja ya kutengeneza video ili tuweze kushoot video kadhaa huku huku.Pia nafanya mawasiliano na wanamuziki mbalimbali kutoka nchi nyingine duniani ili kubadlishana mawazo na pia kuangalia uwezekano wa kufanya kazi pamoja.

Mbali na yote hayo,kama unavyofahamu mimi ni Balozi wa MARALIA NO MORE.Wao pia wametumia nafasi hii kunialika New York yalipo makao yao makuu.Nitakuwa huko tarehe 28 na 29 July ili nikutane na staff wote kwa pamoja.Vyombo kadhaa vya habari vitakuwepo na hivyo bila shaka kutakuwa na media coverage.

BC: Kama Balozi wa Malaria No More,unaonaje kuhusiana na vita dhidi ya ugonjwa huo nchini kwetu? Utakuwa na ujumbe wowote maalumu utakapokutana na staff nzima ya Malaria No More?

PROF.JAY: Kwa kweli jitihada za kupambana na ugonjwa wa malaria zinakwenda vizuri.Kwa kutumia muziki,wananchi wengi wamepata nafasi ya kuelewa jinsi ugonjwa huo unavyoenea,mbinu za kupambana nao nk.

Nitakapokutana na staff wa Malaria No More,nitawaeleza zilipofikia jitihada zetu na jinsi tulivyofanikiwa kuwazindua watanzania kuhusiana na ugonjwa huu hatari ambao unaua mamilioni ya watanzania kila mwaka huku wengi wao wakiwa ni watoto chini ya miaka mitano(5) na akina mama wajawazito. Jitihada hizi zinaendelea kufanikiwa kutokana na mchango na support kubwa kutoka kwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete.

BC: Je unatarajia kutoa albamu mpya mwaka huu? Kama sivyo,lini mashabiki wako watarajie album mpya?

PROF.JAY: Ni kweli,it’s about time.Hopefully ambo yote yakienda sawa mwakani mwanzoni nitatoa album mpya. Kwa hiyo mashabiki wangu vuteni subira kidogo. Kazi tumeshazi-record ila tunachozingatia ni lini muda muafaka wa kuzitoa.Nasubiri muongozo kutoka kwa Management yangu.

BC: Shukrani Prof.Tunakutakia kila la kheri katika American Tour yako.

PROF.JAY: Asanteni sana wakuu.


Unaweza kuwaita FFU ukipenda.Lakini ukiwatambua au kuwatambulisha kama The Ngoma Africa Band,unakuwa hujakosea pia.Ni bendi inayoundwa na watanzania yenye makao yake makuu nchini Ujerumani.

Katika kuendeleza shamrashamra za majira ya kiangazi(summer), Jumamosi tarehe 7 mwezi wa Nane(August) vijana hao machachari watakuwepo jijini Frankfurt,huko huko Ujerumani katika tamasha kubwa linalojulikana kama Afrika & Karibik Festival litakalofanyika katika viwanja vya Robestock Park hapo Frankfurt.

Baada ya hapo FFU hao wanatarajiwa kuwasha moto katika tamasha lingine kubwa mjini Keiserslautern,Ujerumani.Hiyo itakuwa siku ya Jumapili tarehe 8-08-2010.

Kazi kwenu mashabiki wa muziki mliopo Frankfurt na Keiserslautern.Msikose kwenda kuwaunga mkono mabalozi hawa wa Tanzania kupitia muziki.

Unaweza kuwasikiliza The Ngoma Africa Band hapa www.myspace.com/thengomaafrica

August is around the corner.That means,our Miss Universe,Hellen, is just few days away before getting on stage to proudly represent our beloved land Tanzania on 23rd August 2010 in Las Vegas,USA. We all want her to win,right? I believe we do.Now to help her do that,we gotta do something considerably small but BIG in helping her win.Vote

To vote for Hellen,kindly go to http://www.missuniverse.com/members/contestants

Go to Hellen’s photo and vote. Thank You.

You can read our recent interview with Hellen by clicking on this link.

KFG LTD- 15th July 2010- Announces the Launch of “African Queen Kanga Jeans”

A hot wind blows in New York. It comes from Africa. It doesn’t however bring sultry equatorial temperatures, but the seeds of new ideas. Vida Mahimbo comes from the slopes of the Kilimanjaro in Tanzania with her collection of Kanga Jeans and a story of synergies between antique and modern, and west and south of the world.

She grew up in the midst of her mother’s looms, listening to the stories her father told when returning from his overseas job as a textile engineer. From this, even when still young, came a personal elaboration of the traditions of her homeland and technological innovations in order to dress the woman of the New Millennium.

After graduating in Business Administration and Marketing at Dar es Salaam, convinced that economic planning is an indispensable requisite for an African stylist, Vida finally created the Karisma Fashion Group, an Italian/Tanzanian business that unites African creativity and the high quality of Italian fabrics. Colours, designs, symbols inspired by Masai culture, combined with forms that reject the sanctioned idea of an ethereal female and proudly show the beauty of real, live bodies, have crossed the confines of Africa and landed in Monte Carlo and Paris boutiques. (more…)

Mkurugenzi Mtendaji wa Global Publishers & General Enterprises Ltd na mjasiriamali, Bw. Eric Shigongo(pichani), anatarajiwa kuhutubia nchini Marekani katika Mkutano maalum ulioandaliwa na Watanzania waishio nchini humo (Diaspora Council of Tanzanians in America – DICOTA).

Katika mkutano huo unaotarajiwa kufanyika kwa muda wa siku nne kuanzia Julai 1, mwaka huu katika jiji la Minneapolis, Marriott Hotel, Minnesota, Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mh. Aman Abeid Karume, amealikwa kuwa mgeni rasmi. Viongozi wengine watakaohudhuria mkutano huo ni pamoja na maofisa waandamizi na wafanyabishara wakubwa kutoka Serikali ya Tanzania na Marekani.

Aidha, Mwenyekiti Mtendaji wa makampuni ya IPP, Bw. Reginald Abraham Mengi, naye ni miongoni mwa wageni waalikwa wa mkutano huo ambao unafanyika kwa mara ya pili nchini humo ukiwakutanisha Watanzania waishio ughaibuni. Mada mbalimbali zitatolewa na Watanzania waishio ndani na nje ya Marekani.

Katika mkutano huo, Bw. Shigongo anatarajiwa kutoa mada itakayoelezea jinsi ya kufanikiwa kiuchumi katika mazingira ya Tanzania na anatarajiwa kuwahamasisha Watanzania waishio ughaibuni kuwekeza nyumbani Tanzania.

Katika siku za hivi karibuni, Bw. Shigongo amejipatia umaarufu kwa kutoa elimu, ushauri kwa vijana na wanafunzi wa shule za msingi, sekondari na vyuo vikuu nchini kupitia mikutano na hafla mbalimbali anazoandaa au kualikwa kwa lengo la kutoa elimu ya ujasiriamali kwa vijana wa kitanzania.

Kwa taarifa zaidi juu ya mkutano huo tafadhali tembelea ukurasa wa Diaspora Council of Tanzanians in America-DICOTA)

Flaviana Matata

Hasheem Thabeet

Former Miss Universe Tanzania 2007, Flaviana Matata and Current NBA Player Hasheem Thabeet Recognized as the Newest Diamond Empowerment Fund Africa’s Angel Ambassador and Athlete For Africa Member. For more information,Click here.

BC: Hongera nyingi kwenu Flaviana na Hasheem.You make us proud!All the best.

Imeandikwa na Na Angela Semaya wa Habari Leo

MAISHA yake sasa yamebadilika, amelazimika kuwa mtumwa wa kujificha kwa kuvaa vazi aina la Hijab ambalo anasema kwake limegeuka kuwa vazi analoliheshimu na kulithamini kwa kuwa ndio msiri wake mkubwa siku hizi, hii yote ni gharama inayotokana na moyo wake wa ujasiri na ushupavu uliotokana na kutumia kalamu yake kufichua uovu na unyanyasaji dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi kwa kuuawa kwa imani za kishirikina.

Kwa walio wengi ndani na nje ya Tanzania, jina la Vicky Ntetema sio geni masikioni mwao kwani ni mwandishi mahiri wa Idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC).

Ntetema aliyezaliwa miaka 51 iliyopita ameibuka kuwa mwandishi mahiri, jasiri na shupavu baada ya kufichua siri ya kutisha kutokana na uchunguzi wa mauaji ya albino na familia zao akitaka kujua kwa undani sababu hasa za mauaji na ukatili dhidi ya albino. Hatimaye kazi yake hiyo imemuwezesha kupata Tuzo ya Ujasiri katika fani ya Uandishi wa Habari inayotolewa na International Women’s Media Foundation.

HABARI LEO Jumapili iliamua kumtafuta Vicky baada kutaka kufahamu kwa undani wa kilichomsukuma kufuatilia habari hiyo na kwa kiwango gani amefanikiwa, maisha yake kwa ujumla na kuhusiana na tuzo hiyo.

Ntetema ambaye alifanya uchunguzi wake kwa siri bila woga anasema Novemba, 2007 alipokea ujumbe wa maneno ukimuelezea kuhusu matukio ya kuuawa albino na kukatwa viungo vyao kwa imani za kishirikina, lakini awali naye hakuamini kama hicho kitu kinawezekana.

Na baada ya kufuatilia kwa muda na kujithibitishia habari hizo, alianza kuishawishi BBC, lakini walionekana kusitika wakiwa na mashaka kwamba kweli inawezekana kuwepo kwa matukio hayo? Hata hivyo anasema hakukata tamaa aliwasiliana na waandishi wengine walioko katika maeneo husika nao walimsaidia kuchunguza na kumpa taarifa zaidi.

Wakati akiendelea na uchunguzi wake aligundua kuwa waganga wa kienyeji ndio waliokuwa wakisababisha mauaji ya albino kwa kuwaambia wateja kuwa wanaweza kupata utajiri kwa kutumia viungo vya walemavu hao, ndipo alipoamua kuishawishi tena BBC huku akiendelea na uchunguzi wake kwa njia ya simu kwa kuwasiliana na watu wa Kanda ya Ziwa.

Kile alichokuwa amekusudia kukifanya na kukifichua, kilithibitishwa na Rais Jakaya Kikwete ambaye Mwezi Machi, 2008 alikemea vitendo hivyo vya kikatili dhidi ya albino na kuweka wazi kuwa tayari watu 19 walishauawa.

“Baada ya Rais kutangaza hivyo, nikasema kama kiongozi wa nchi amekemea kiasi hili na ametaja hadi maeneo yanayohusika na matukio hayo…kwa sababu ya kuwa na uhusiano mzuri na wahariri nilipeleka maombi yangu bila kusita wanisaidie ili niweze kwenda kabisa eneo husika ingawa waliniambia kwa kipindi hicho hawakuwa na bajeti,” anasema.

Dhamira yake ilimsukuma Ntetema kuchukua fedha zake za mshahara na kuamua kwenda Mwanza kwa ajili ya kuendelea na uchunguzi wake. Anasema kazi hiyo ilimlazimu kuzunguka sehemu mbalimbali hadi akajikuta ameishiwa fedha na kulazimika kuomba kwa mama yake. (more…)

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page