MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

Josefina Nunez, Miss British Virgin Islands 2010; Qory Sandioriva, Miss Indonesia 2010; and Hellen Dausen, Miss Tanzania 2010, pose in their Dar Be Dar swimsuits during the registration and fitting process in preparation for the Miss Universe 2010 Competition at Mandalay Bay Hotel and Casino in Las Vegas, Nevada on Sunday, August 8, 2010. The Miss Universe 2010 competition that will air live on the NBC Television Network at 9 PM ET, August 23, 2010

Wapenzi wa burudani, hususani ya muziki, wa jijini Dar-es-salaam na sehemu mbalimbali za Tanzania,jumamosi ijayo wanatarajia kupata burudani ya aina yake wakati wa kilele cha tamasha la Fiesta kwa mwaka 2010.

Kwa miaka kadhaa sasa,Fiesta limekuwa ni tamasha ambalo husubiriwa kwa hamu na watanzania hususani wanaopenda mambo ya kujichanganya au kujipa raha.

Mbali na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali wanaotamba nchini,tamasha hilo limekuwa likiwapa wapenzi wa muziki nchini Tanzania kuwaona baadhi ya wanamuziki wanaotikisa katika nchi mbalimbali ulimwenguni likiwemo taifa la Marekani ambalo limesheheni wanamuziki wanaotamba ulimwenguni kote.

Katika kuendeleza utamaduni huo wa kuwaleta wanamuziki wa kimataifa,Fiesta ya mwaka huu itawapa wapenzi wa burudani nafasi ya kuwaona jukwaani wasanii kama vile Lil Kim kutoka Marekani,Bracket kutoka Nigeria na jamaa wa “Aladji” kutoka Ivory Coast na mtindo wa Coupé Décalé.

Fiesta ya mwaka huu kwa jiji la Dar-es-salaam itafanyikia katika Viwanja vya Leaders Club,Kinondoni jijini Dar-es-salaam.Kazi kwenu wapenzi wa kujirusha.

Lil Kim kutoka USA.Mwanadada huyu ana historia ndefu sana katika muziki wa Rap/Hip Hop.Alikuwepo na bado yupo.

Bracket kutoka Nigeria.Hawa jamaa wametamba sana na wimbo wao Yori Yori ambao wanasema unaweza kuwa na maana nyingi.

From Ivory Coast

Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Prof.Jay,bado anaendelea na tour yake ndani ya USA.Hapo jana ilikuwa zamu ya watu wa Washington,DC kupata burudani kutoka kwa msanii huyo.Mambo yote yalifanyikia ndani ya sehemu maarufu ijulikanayo kama Zanzibar.

Wikiendi ijayo ni zamu ya watu wa Boston,Massachusetts.

Prof.Jay jukwaani.

An admiration look.Can you spot it?

People showed up and had a good time.

Prof.Jay,The Heavy Weight MC

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Unapoongelea wanamuziki wa muziki wa kizazi kipya ambao miziki yao na mashairi yao yametoa mchango mkubwa katika kuufanya muziki huo ukubalike na kupewa heshima na nafasi yake katika jamii,bila shaka huwezi kuthubutu kumweka pembeni Joseph Haule au kama anavyojulikana miongoni mwa washabiki na wadau wa muziki; Proffessor Jay,MC Shupavu,The Heavy Weight MC,Jay wa Mtulinga,Mti Mkavu,Jiizeh nk.

Hivi sasa Prof.Jay yupo nchini Marekani akiendelea na tour yake ndani ya taifa hilo ambalo hivi sasa linaongozwa na Barack Obama,Rais wa kwanza mweusi. BC ilipata nafasi ya kufanya naye mahojiano kuhusiana na ziara hiyo. Je unataka kujua atatua na kufanya shows katika miji na majimbo gani? Anasemaje kuhusu ambacho ameweza kukiona na kujifunza nchini humo mpaka hivi sasa? Kwa majibu ya maswali hayo na mengine,fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo;

BC: Prof,asante kwa nafasi hii ya mahojiano mafupi.Mambo yanakwendaje?

PROF.JAY: Safi vipi mtu wangu?Na mimi nashukuru kwa kunipa nafasi hii adimu.

BC: Ni muda sasa umekuwa nchini Marekani kwa ajili ya American Tour yako kiasi kwamba mashabiki wako ambao hawajui uko wapi wamekuwa wakijiuliza maswali yasiyo na majibu ya haraka.Kupitia hapa BC unaweza kuwaeleza kwa sasa hapo Marekani makazi yako ni katika State au Jimbo gani?

PROF.JAY: Asante na naomba niseme samahani kwa wale ambao wamekuwa wakijiuliza kwamba nipo wapi na mambo kama hayo.Kwa sasa hapa nchini Marekani nipo Massachussets nikiwa nimeweka kambi na DJ wangu anayekwenda kwa jina la RICHMAKA.Na sababu ya kuweka kambi hapa ni ili kupata muda wa kutosha wa kufanya mazoezi kwa pamoja kama team ili shows ninazofanya ziwe katika kiwango cha hali ya juu na mashabiki wangu wapate thamani halisi ya pesa zao watakazotoa ili kuja kwenye shows.

BC: Ni kampuni gani inakusimamia katika hii tour yako hapo nchini Marekani?

PROF.JAY: Kampuni inayonisimamia inaitwa NGOME ENTERTAINMENT.Makao yake makuu yapo Dallas,Texas.Kampuni hii ipo chini ya CEO wake,Kitova Mungai.

BC: Ni miji gani ambako unatarajia kuwa na shows?

PROF JAY: Mpaka hivi sasa nimeshapiga show moja ambayo ilifanyikia pale Houston,Texas tarehe 4 Julai(siku ya kusheherekea Uhuru hapa nchini Marekani) Ratiba ya shows zinazofuatia ni kama ifuatavyo:

  • Tarehe 31/8/2010 Washington,D.C
  • Tarehe 7/8/2010 Boston,Massachusetts.
  • Tarehe 13/8/2010 Dallas,Texas.
  • Tarehe 19/8/2010 Kansas City,Missouri.
  • Tarehe 20/8/2010 Witchita,Kansas.
  • Tarehe 11/9/2010 Atlanta,Georgia.

Mpaka hivi sasa ratiba ndio hiyo. Lakini kuna shows zingine nyingi ambazo zinaweza kutokea kwa sababu Promoters kadhaa wameonyesha nia na kufanya majadiliano ya awali ingawa hatuja-confirm firm tarehe kamili za kufanya kazi. Pia naomba niweke wazi kwamba milango ipo wazi kwa promoters wengine ambao wanataka kubook shows.Wenye nia hiyo wanaweza kuwasiliana na Kitova kwa kutumia nambari ya simu +1 214 455 5082 au DJ Rich Maka kwa nambari +1 413 262 0400.Karibuni sana.

BC: Unawaambia nini mashabiki wako katika miji hiyo?Watarajie nini kutoka kwako?

PROF.JAY: Kama nilivyogusia hapo juu,mashabiki wategemee shows za kiwango cha juu kabisa ambayo hawajawahi kuiona kutoka kwa msanii yeyote kutoka kwenye ukanda wa Afrika Mashariki,kati na Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Ninachowaomba wajitokeze kwa wingi ili wasije wakayakosa yale niliyowaandalia.Pia nawaomba wapatapo habari hii wawaambie na wengine.

BC: Waswahili wanasema kutembea kwingi ni kuona mengi pia.Mpaka hivi sasa unaweza kusema umejifunza nini kutokana na ambacho umekiona nchini Marekani iwe ni kwa upande wa sanaa ya muziki au jamii kwa ujumla?

PROF.JAY: Kwanza kabisa nimejifunza professionalism. Huku watu wanaheshimu sana kazi zao. Muda wa kazi ni muda wa kazi. Pia muziki wa huku upo katika kiwango cha juu. Bila shaka na sisi tunahitaji marekebisho mengi sana ili nasi tuboreshe miziki yetu na kazi zetu za sanaa zifikie angalau robo tatu ya kiwango ambacho wenzetu wameshafikia.Nasema hivyo kwa sababu huku muziki ni kazi na ni ajira kubwa sana kwa vijana na hata wasio vijana.Inaheshimika kama kazi nyingine zingine zozote.

Kila anapofanya show,umati kumbi na viwanja huwa “vinatapika”.Hapo ilikuwa ndani ya CCM Kirumba-Mwanza.Can you do a count from this photo?

BC: Baada ya Tour yako nchini Marekani unatarajia kuelekea katika nchi nyingine kuendelea na tour au utarudi kwanza nyumbani kupumzika kidogo?

PROF.JAY: Baada ya kukamilisha hii tour,nitarudi nyumbani kwa mapumziko mafupi kisha nitaelekea Ulaya kwa tour nyingine.Mpaka sasa nimeshapata mwaliko kutoka nchi za Scandinavia(Sweden,Norway,Denmark na Finland).Pia nimepata mwaliko wa kwenda kutumbuiza nchini Uingereza. Nitakaporudi nyumbani ndio nitajua wapi pa kuanzia.Mashabiki na wadau watajulishwa kuhusu tour hizo kupitia vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo BongoCelebrity.

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

BC: Mbali na hiyo tour kuna shughuli nyingine unafanya huko Marekani?

PROF.JAY: Ni kweli kabisa.Mbali na tour pia narekodi miziki.Tumeshaongea na kampuni moja ya kutengeneza video ili tuweze kushoot video kadhaa huku huku.Pia nafanya mawasiliano na wanamuziki mbalimbali kutoka nchi nyingine duniani ili kubadlishana mawazo na pia kuangalia uwezekano wa kufanya kazi pamoja.

Mbali na yote hayo,kama unavyofahamu mimi ni Balozi wa MARALIA NO MORE.Wao pia wametumia nafasi hii kunialika New York yalipo makao yao makuu.Nitakuwa huko tarehe 28 na 29 July ili nikutane na staff wote kwa pamoja.Vyombo kadhaa vya habari vitakuwepo na hivyo bila shaka kutakuwa na media coverage.

BC: Kama Balozi wa Malaria No More,unaonaje kuhusiana na vita dhidi ya ugonjwa huo nchini kwetu? Utakuwa na ujumbe wowote maalumu utakapokutana na staff nzima ya Malaria No More?

PROF.JAY: Kwa kweli jitihada za kupambana na ugonjwa wa malaria zinakwenda vizuri.Kwa kutumia muziki,wananchi wengi wamepata nafasi ya kuelewa jinsi ugonjwa huo unavyoenea,mbinu za kupambana nao nk.

Nitakapokutana na staff wa Malaria No More,nitawaeleza zilipofikia jitihada zetu na jinsi tulivyofanikiwa kuwazindua watanzania kuhusiana na ugonjwa huu hatari ambao unaua mamilioni ya watanzania kila mwaka huku wengi wao wakiwa ni watoto chini ya miaka mitano(5) na akina mama wajawazito. Jitihada hizi zinaendelea kufanikiwa kutokana na mchango na support kubwa kutoka kwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete.

BC: Je unatarajia kutoa albamu mpya mwaka huu? Kama sivyo,lini mashabiki wako watarajie album mpya?

PROF.JAY: Ni kweli,it’s about time.Hopefully ambo yote yakienda sawa mwakani mwanzoni nitatoa album mpya. Kwa hiyo mashabiki wangu vuteni subira kidogo. Kazi tumeshazi-record ila tunachozingatia ni lini muda muafaka wa kuzitoa.Nasubiri muongozo kutoka kwa Management yangu.

BC: Shukrani Prof.Tunakutakia kila la kheri katika American Tour yako.

PROF.JAY: Asanteni sana wakuu.


Unaweza kuwaita FFU ukipenda.Lakini ukiwatambua au kuwatambulisha kama The Ngoma Africa Band,unakuwa hujakosea pia.Ni bendi inayoundwa na watanzania yenye makao yake makuu nchini Ujerumani.

Katika kuendeleza shamrashamra za majira ya kiangazi(summer), Jumamosi tarehe 7 mwezi wa Nane(August) vijana hao machachari watakuwepo jijini Frankfurt,huko huko Ujerumani katika tamasha kubwa linalojulikana kama Afrika & Karibik Festival litakalofanyika katika viwanja vya Robestock Park hapo Frankfurt.

Baada ya hapo FFU hao wanatarajiwa kuwasha moto katika tamasha lingine kubwa mjini Keiserslautern,Ujerumani.Hiyo itakuwa siku ya Jumapili tarehe 8-08-2010.

Kazi kwenu mashabiki wa muziki mliopo Frankfurt na Keiserslautern.Msikose kwenda kuwaunga mkono mabalozi hawa wa Tanzania kupitia muziki.

Unaweza kuwasikiliza The Ngoma Africa Band hapa www.myspace.com/thengomaafrica

Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Angeris,akitoa burudani ya aina yake wakati wa Tamasha la kila mwaka la Fiesta.La mwaka huu limepewa jina la Fiesta Jipanguse. Hiyo ilikuwa Zenji wikiendi iliyopita.

Kwa picha chungu tele juu ya Tamasha hilo,Michuzi Jr,anakukaribisha uzicheki kwa kubonyeza hii link.

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page