
Ukumbi umefurika,watu wananyanyua na kushusha mikono.Wanaimba na kucheza.Wengi wamevalia nguo nyekundu.Siku ya siku ni Valentine’s Day au Siku ya Wapendanao.Kila mtu na wake. Ni siku ya kumuonyesha mwenzako kwamba unampenda.Kama alikuwa haamini huenda leo akaamini.Mwanamuziki aliyepo jukwaani ni TID.Mahali ni Platinum Club,Mikocheni.
Ghafla muziki unazimwa.TID anasema kuna kitu anataka sema.Waungwana wakatulia ili kumsikiliza.Anaanza kuongea “Wapendwa, muda umewadia,nataka kuuaga ukapela.Nataka kuoa”. Watu kimyaa, minong’ono ya chini kwa chini,shauku ya kutaka kujua na kusikiliza zaidi!
Kwa mujibu wa John Bukuku wa Full Shangwe,kilichofuata ni TID kumtambulisha mchumba.Anaitwa Kinana(pichani). TID akapiga goti na kutamka “Will You Marry Me”? Binti akakubali.TID and Kinana are engaged.
Hongera TID.Maisha ni hatua.Tunasubiri harusi.Kila la kheri.
Picha na chanzo cha habari:Full Shangwe.
Kama wewe ni mtizamaji au mpenzi wa sinema za kutoka nchini Nigeria,bila shaka umewahi kuwaona wachekeshaji wawili wajulikanao kama Aki na Ukwa.Wanasemekana ndio waigizaji wafupi kuliko wote nchini humo.Habari nzuri,kama wewe unapendezwa na vichekesho vya Aki na Ukwa ni kwamba wapo njiani kuja jijini Dar-es-salaam.
Kwa mujibu wa Gazeti la Mwanaspoti,wachekeshaji hao wanatarajiwa kufanya vitu vyao katika tamasha la watoto yatima, na wale wanaoishi katika mazingira magumu Februari 14 mwaka huu. Tamasha hilo linatarajiwa kufanyika siku ya wapendanao(Valentine’s Day) katika viwanja vya TTCL, Kijitonyama jijini Dar es salaam.
Aki na Ukwa watakuwa nchini kwa lengo wa kucheza na kufurahi na watoto mbalimbali wahishio kwenye mazingira magumu.
Watasindikizwa na wasanii wengine wa ndani wanaotarajiwa kutumbuiza katika tamasha hilo ni pamoja na Ze Comedy, Q-Chief, Mr.Nice, Rose Mhando na Mrisho Mpoto. Kwa habari zaidi bonyeza hapa.

Miongoni mwa matukio ya ki-muziki ambayo yataendelea kukumbukwa kwa muda mrefu ni pamoja na tukio la jumla ya wanamuziki 45 kukusanyika katika studio za Jim Henson za jijini Los Angeles mwaka 1985 na kutengeneza wimbo ulioitwa We Are The World ambao ulikuwa mahsusi kwa kuchangia fedha kwa ajili ya Afrika na hususani nchi ya Ethiopia ambayo ilikuwa imekumbwa na ukame wa kutisha kuanzia mwaka 1984-1985.Ulikuwa ni umoja na upendo wa aina yake waliouonyesha wanamuziki wale sio tu kwa bara la Afrika bali kwa taasisi nzima ya ubinadamu. Wanamuziki Lionel Richie na Michael Jackson(RIP) ndio walioandika wimbo ule ambao ulifanikiwa kuchangisha jumla ya dola milioni 30 zilizokwenda kusaidia waathirika wa ukame ule.
Katika kujaribu kurudia kile walichofanya superstars wa ulimwengu wa muziki takribani miaka 25 iliyopita, hapo juzi jumla ya wasanii 100 (wengi wao kutoka Marekani) ambao wanatamba hivi sasa katika muziki ulimwenguni,walikusanyika katika studio moja chini ya Producer yule yule aliyefyatua We Are The World ya mwaka 1985,Quincy Jones ili kuutengeneza upya wimbo wa We Are The World(remake of We Are The World). Lakini safari hii sio kwa ajili ya kuchangia Afrika bali ndugu zetu wa Haiti ambao kama unavyojua wiki chache zilizopita nchi yao ilipata tetemeko la ardhi ambalo linahofiwa kwamba lilichukua maisha ya jumla ya watu 200,000.
Original We Are The World.
Baadhi ya wanamuziki wenye majina makubwa ambao wamo katika We Are The World mpya ni pamoja na Wyclef Jean, Kanye West,Celine Dion,Jennifer Hudson,Miley Cyrus,Barbra Streisand,Tony Bennett,Jamie Foxx,Natalie Cole, Akon, Carlos Santana,Josh Groban,Justin Bieber(kijana wa miaka 15 raia wa Canada,alikuwa hajazaliwa huyu mwaka 1985), Snoop Dogg,Drake,LL Cool J na hata Rapper Lil Wayne ambaye anasema alidhani wanamtania alipoambiwa kwamba anahitajika “kuimba”.
Wengine ni kama vile Usher,Jonas Brothers,Pink, Gladys Knight,Wil.i.am,Brandy,Keri Hilson,Busta Rhymes,T-Pain,Robin Thicke,Trey Songz,Adam Levine,Tyrese na wengine kibao.Nitaendelea kuongeza majina ya washiriki wengine katika orodha hii kwa kumbukumbu ya vizazi vijavyo.
Janet Jackson(dada wa Michael Jackson) ambaye hakuwepo studio anatarajiwa kuimba sehemu ya marehemu kaka yake kabla ya kutolewa rasmi kwa video ya remake hii ya We Are The World ambayo inatarajiwa kuonyeshwa rasmi tarehe 12 mwezi huu katika kituo cha televisheni cha NBC cha nchini Marekani kwenda sambamba na ufunguzi wa michezo ya Olympics ya majira ya baridi(Winter Olympics) inayofanyikia huko Vancouver nchini Canada kwa mwaka huu. Video ya wimbo huu mpya imeongozwa na Director wa movie ya Crash(kama hujaiona fanya bidii uione),Paul Haggis.
Je unadhani kuna uwezekano wa wimbo huu uliotengenezwa upya,kuushinda ule wa zamani au kupata mafanikio zaidi ya original? Kuna watu wanasema ni vyema kwamba Lionel Richie na Quincy Jones wapo kusimamia na kuhakikisha kwamba the “1985 spirit ” inabakia pale pale lakini bila kuwepo kwa Michael Jackson ni pengo kubwa sana.Wewe unasemaje?
Photo/Kevin Mazur/wireimage.com. Kwa picha zaidi bonyeza hapa.
Tuzo maarufu za muziki za Grammy zimemalizika muda mfupi uliopita jijini Los Angeles.Kama kawaida ya tuzo maarufu kama hizo,huwa kuna kuvunjwa kwa rekodi au kuwekwa rekodi mpya,vituko mbalimbali, mavazi ya kukumbukwa na pia performances za kukumbukwa.
Kwa mwaka huu,rekodi mpya imewekwa na Beyonce Knowles.Binti huyo ambaye ni mke wa rapper maarufu ulimwenguni,Jay-Z ameibuka na jumla ya tuzo sita na hivyo kuweka rekodi ya kuwa mwanamuziki wa kike wa kwanza kushinda idadi hiyo ya tuzo katika usiku mmoja wa tuzo za Grammy!
Kwa upande wa performances ambazo nitazikumbuka kwa muda ni pamoja na performance aliyofanya Pink huku akijibinubinua hewani kwa kutumia kipande cha nguo! Kuna haja ya kuchunguza zaidi ili kujua kiasi gani cha ile performance ni kweli na kiasi gani ni uzushi.It was hot though.
Nyingine niliyoipenda ni performance ya Lil Wayne(yuko mbioni kwenda jela kwa miezi nane na huenda hii ilikuwa ni performance yake ya mwisho), Drake na Eminem. Nilifurahi kumuona Eminem akiwa bado yupo fit na huku uwezo wake wa kumiliki jukwaa ukiwa pale pale.Hapo katikati alipotea kutokana na matumizi ya kutisha ya madawa ya kulevya.
Mavazi: Mimi sio mtaalam sana wa mambo ya mavazi.Lakini hata hivyo hiyo haikunizuia kuona kwamba Lady Gaga alitia fora kwa kivazi alichovaa baada ya ku-perform na kuungana na wenzake katika audience.Sijui bado jina la kitu alichovaa;ni gauni au?
Kwa ujumla tuzo kubwa kubwa zilienda kama ifuatavyo;
- Record of the Year – Kings of Leon – “Use Somebody”
- Album of the Year – Taylor Swift – ‘Fearless’
- Song of the Year – Beyonce – “Single Ladies (Put a Ring On It)”
- Best New Artist – Zac Brown Band
- Best Female Pop Vocal – Beyonce – “Halo”
- Best Male Pop Vocal – Jason Mraz – “Make It Mine”
- Best Duo or Group With Vocals – Black Eyed Peas – “I Gotta Feeling”
- Best Pop Vocal Album – Black Eyed Peas – ‘The E.N.D
Kwa orodha kamili ya washindi,bonyeza hapa.

Mashabiki wa muziki,hususani wa R&B waliopo katika ukanda wa Afrika Mashariki na hususani jijini Kampala nchini Uganda,huenda kesho wakashuhudia onyesho ambalo hawajashuhudia ndani ya miaka kadhaa na huenda wasishuhudie katika miaka kadhaa ijayo.Hiyo ni ahadi,sio kutoka kwangu bali kutoka kwa mwanamuziki Robert Sylvester Kelly maarufu kama R.Kelly(pichani) kutoka nchini Marekani anayetarajiwa kufanya onyesho la aina yake hapo kesho jijini Kampala katika ukumbi wa Lugogo Cricket Oval.
Onyesho hilo ambalo limedhaminiwa na kampuni ya simu ya Zain,limepewa jina la “I Believe”.Hivi karibuni iliarifiwa kwamba kampuni ya Zain imetumbukiza zaidi ya $2.5 kwa ajili ya onyesho hilo kwani inasemekana kwamba kwa R.Kelly kukubali kufanya show yoyote nje ya Amerika Kaskazini basi $600,000 lazima ziwe mezani. Viingilio katika onyesho hilo ambalo tiketi zake zilishakwisha(sold out) wiki mbili zilizopita, vimepangwa kuwa Ushs 30,000(Silver) Ushs 125,000(Gold) na Ushs 250,000(Platinum). Hii ni mara ya kwanza kwa R.Kelly kufanya concert katika ukanda wa Afrika Mashariki. Na barani Afrika kwa ujumla mahali pengine ambapo amewahi kufanya onyesho ni Afrika Kusini tu.
R.Kelly ameahidi kuimba nyimbo zake zote ambazo amewahi kutamba nazo kama vile Bump n’Grind, I Believe I Can Fly,Gotham City,Ignition(Remix),The World’s Greatest,If I could turn back the hands of time, na nyinginezo tele bila kusahau hip-hopera yake ya Trapped In A Closet.
Sasa kwa wale ambao mmeshawahi kuhudhuria show yeyote ya R.Kelly,mnajua kwamba yeye hupenda mashabiki wanaokwenda naye sambamba.Hupenda kuwashirikisha hadhira(audience).Kazi kwenu.Jukwaani R.Kelly anatarajia kusindikizwa na wasanii wa Uganda Bebe Cool,Jose Chameleon,GNL,Peter Miles na Goodlyf ambao ni Radio na Weasel.Wote hao wamepigiwa kura na waganda wenyewe ili kupata nafasi hiyo.
Here is one my favourite from him; Step In The Name Of Love.

Binti au mrembo unayemuona pichani anaitwa Lilian Mduda(21). Huyu ndiye mwakilishi wetu katika fainali za shindano la kumsaka Kisura wa Afrika kupitia Mnet(Mnet Face of Africa) zinatarajiwa kufanyikia jijini Lagos nchini Nigeria tarehe 6 Februari/2010. Jumla ya warembo 10 kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika ndio waliofanikiwa kuingia katika fainali hizo na kwa maana hiyo ndio wataochuana.
Warembo wengine waliofanikiwa kufikia fainali wanatoka katika nchi za Angola,Ethiopia,Ghana,Kenya,Mozambique,Nigeria,South Africa,Zambia na Zimbabwe.
Lilian Mduda ambaye ni mwanfunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam akisomea Biashara(B.Comm), amesema amejiandaa vyema kwa ajili ya shindano hilo na haoni mshiriki yeyote anayemtisha isipokuwa ni yeye mwenyewe anayeweza kujiwekea mazingira ya kushinda kwa kuzingatia yale yote atakayoelekezwa na kuyafanya kwa ufanisi ili aweze kufikia malengo yake katika fainali hizo.
Lilian anapenda kusoma novels zenye hadithi za kimapenzi na chakula akipendacho ni wali na maharage.Ndoto zake ni pamoja na kuweza kutembelea jiji la Paris siku moja.Pia anapenda mpira wa kikapu(basketball) na hupenda kusikiliza mziki na kujisomea.Kila la kheri Lilian.
Ukitaka kujua zaidi kuhusu Mnet Face of Africa na warembo wengine wanaoshiriki,bonyeza hapa.

Visura 12 wa M-Net wanaowania nafasi ya kuchuana kwenye fainali za kumtafuta kisura wa Africa(M-Net Face of Africa) zitakazofanyika katika jiji la Lagos, Nigeria, Februari 6, 2010.

Ijumaa hii katika ukumbi wa Mlimani City,ni kivumbi na jasho.Mrembo wa Afrika Mashariki atakuwa akitafutwa. Zawadi kuu ni Toyota Celica Sports kama inavyoonekana pichani juu na huku warembo wanaowania taji hilo wakiwa wamelizunguka.
Nani atalinyakua gari hilo?Hilo ndilo swali la msingi. Kwa picha zaidi za warembo hao,na habari zaidi kuhusu tukio hili,bonyeza hapa.

Kwa mara nyingine tena, Tanzania imetoka patupu katika kuwania taji la Miss World. Taji la mwaka huu limekwenda kwa mrembo kutoka nchi ndogo ya Gibraltar, Kaiane Aldorino(23). Mashindano ya mwaka huu ambayo yalijaa vionjo vya ngoma na wanenguaji wa kiasili,zilifanyikia nchini Afrika Kusini.
Nafasi ya pili ilikwenda kwa Miss Mexico,Perla Beltran Acosta huku ya tatu ikienda kwa Miss South Africa, Tatum Keshwar ambaye ndiye alishangiliwa zaidi pengine kwa kuzingatia kwamba yeye alikuwa anachezea katika “uwanja wa nyumbani”.
Jumla ya washiriki 112 walishiriki katika shindano hilo ambapo Tanzania ilikuwa inawakilishwa na Miriam Gerald mrembo kutoka jijini Mwanza,kaskazini mwa Tanzania.
Ukitaka kujua zaidi kuhusu nchi anayotoka Miss World mpya bonyeza hapa.

BINGWA wa zamani wa masumbwi katika uzito wa juu duniani, Evander Holyfield wa Marekani amepanga kwenda Uganda kuzichapa na Francois ‘White Buffalo’ Botha wa Afrika Kusini.
Kwa mujibu wa waratibu wa pambano hilo la kimataifa, wababe hao watazichapa Januari 16, wakiwania mkanda wa dunia wa WBF.
Pambano hilo ambalo litavuta hisia za wengi, litapiganwa siku hiyo katika Uwanja wa Taifa wa Mandela, mjini Kampala, Uganda. Kwa habari zaidi,bonyeza hapa.

