MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    



Email for bands
Quantcast

Hii ni kutoka kwa DJ Fetty.Wimbo ninaoupenda zaidi ni wa kwanza hapo kutoka kwa kijana anayeitwa Roma.Wimbo ni Mr.President.Mtembelee DJ Fetty kwa kubonyeza hapa.

Mashabiki wa muziki,hususani wa R&B waliopo katika ukanda wa Afrika Mashariki na hususani jijini Kampala nchini Uganda,huenda kesho wakashuhudia onyesho ambalo hawajashuhudia ndani ya miaka kadhaa na huenda wasishuhudie katika miaka kadhaa ijayo.Hiyo ni ahadi,sio kutoka kwangu bali kutoka kwa mwanamuziki Robert Sylvester Kelly maarufu kama R.Kelly(pichani) kutoka nchini Marekani anayetarajiwa kufanya onyesho la aina yake hapo kesho jijini Kampala katika ukumbi wa Lugogo Cricket Oval.

Onyesho hilo ambalo limedhaminiwa na kampuni ya simu ya Zain,limepewa jina la “I Believe”.Hivi karibuni iliarifiwa kwamba kampuni ya Zain imetumbukiza zaidi ya $2.5 kwa ajili ya onyesho hilo kwani inasemekana kwamba kwa R.Kelly kukubali kufanya show yoyote nje ya Amerika Kaskazini basi $600,000 lazima ziwe mezani. Viingilio katika onyesho hilo ambalo tiketi zake zilishakwisha(sold out) wiki mbili zilizopita, vimepangwa kuwa Ushs 30,000(Silver) Ushs 125,000(Gold) na Ushs 250,000(Platinum). Hii ni mara ya kwanza kwa R.Kelly kufanya concert katika ukanda wa Afrika Mashariki. Na barani Afrika kwa ujumla mahali pengine ambapo amewahi kufanya onyesho ni Afrika Kusini tu.

R.Kelly ameahidi kuimba nyimbo zake zote ambazo amewahi kutamba nazo kama vile Bump n’Grind, I Believe I Can Fly,Gotham City,Ignition(Remix),The World’s Greatest,If I could turn back the hands of time, na nyinginezo tele bila kusahau hip-hopera yake ya Trapped In A Closet.

Sasa kwa wale ambao mmeshawahi kuhudhuria show yeyote ya R.Kelly,mnajua kwamba yeye hupenda mashabiki wanaokwenda naye sambamba.Hupenda kuwashirikisha hadhira(audience).Kazi kwenu.Jukwaani R.Kelly anatarajia kusindikizwa na wasanii wa Uganda Bebe Cool,Jose Chameleon,GNL,Peter Miles na Goodlyf ambao ni Radio na Weasel.Wote hao wamepigiwa kura na waganda wenyewe ili kupata nafasi hiyo.

Here is one my favourite from him; Step In The Name Of Love.

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Movie inaitwa Legion. Mungu amekosa imani na wanadamu.Anatuma malaika kuja kuiangamiza dunia. Starring Paul Bettany, Dennis Quaid,Lucas Black,Tyrese Gibson etc.Imeongozwa na Scott Stewart

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Movie inaitwa Extraordinary Measures: Ni kisa cha kweli kinachowahusu wazazi John na Ailleen Crowley ambao wanajitolea kudhamini utatutwaji wa tiba kwa ugonjwa wa nadra ambao unawateketeza watoto wao wawili.Movie nzuri sana hii kwa wazazi.Starring Harrison Ford,Brendan Fraser, Courtney B.Vance nk.Imeongozwa na Tom Vaughan

vijana-jazzbcKama unaishi katika dunia hii hii tuijuayo sote,basi bila shaka umeshawahi kusikia kuhusu ugomvi kati ya mke wa kaka na dada zake kaka.Kwa maneno mengine ugomvi kati ya fulani na wifi yake au wifi yao.Mimi nimeshawahi kusikia na pia kuona mtu na wifi yake ambao hawapikiki chungu kimoja.Kila kukicha “kesi za ukoo” zilikuwa haziishi.Amani hakuna,kila mmoja anadai kuwa malikia wa boma.

Je ni kwanini huwa kunatokea ugomvi ugomvi hivi kati ya mtu na wifi yake au wifi zake?(sio wote lakini.Wapo mtu na wifi yake au zake wanaoiva kupita maelezo) Hili swali pengine limeshaulizwa mara milioni kidogo na bado majibu yasipatikane.Tunaweza kujaribu kutafuta majibu mapya kama tunataka.Mimi sitochangia.Sijui.

Pamoja na hayo, miaka kadhaa iliyopita bendi ya Vijana Jazz walijaribu kulijibu swali hilo katika kibao chao maarufu kilichoitwa Wifi Zangu. Aliyeongoza mashambulizi alikuwa mwanadada Kida Waziri.Nakumbuka kuwaona Vijana Jazz wakiuliza swali hili pale katika Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro enzi hizo.Kwa kweli ilikuwa ni burudani ya aina yake.

Nakuomba usikilize kibao hiki kisha,baada ya burudani, tafakari kisha jaribu kutupa majibu yako.Kwanini unadhani huwa sometimes inatokea rabsha kati ya mtu na wifi yake?Nani alaumiwe?Nakutakia weekend njema.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

** Wimbo huu sio original.Ni remake tu.Pata burudani.

drremmyKwanza kabisa naomba msamaha kwa kutobandika “burudani yetu” ya zilipendwa kila ijumaa kwa takribani wiki mbili mfululizo.Nilikuwa nikibadilisha makazi kidogo.Ule mtaa niliokuwa nikikaa zamani nimehama! Ingawa haukuwa na mapaka yasiyoisha kulia lia kama alivyoimba Mwaruka katika wimbo wake Mtaa wa Saba, kuhama ilibidi.

Ni ijumaa tena.Kwa wale wanaoishi katika zile nchi zinazokuwa na majira maarufu ya “summer”, ni wakati mwingine wa kutoka nje,kuota jua na pia kutizama miili! Huu huwa ni wakati wa wazimu hususani kwa wenzetu wanaoitwa “weupe”(kuna mtu mweupe duniani?). Ukiwa na mambo ya mfadhaiko basi jikalie tu nyumbani mtu wangu.

Lakini hata sisi bongo tunayo majira yetu ya summer ingawa badala ya joto kali sisi huwa tuna kijiubaridi fulani hususani ile mikoa ya kaskazini na nyanda za juu kusini.Unajua tena,sisi tunachojali ni jina tu na wala sio hali halisi.Ukisema summer time tu kwetu inatosha.Usilete za kuleta.

Maneno pembeni,nyanyuka tucheze. Nani mwingine wa kutunyanyua vitini kucheza zaidi ya Dr.Remmy Ongala na Orchestra Matimila? Msikilize hapa akimlilia Mariamu wake katika wimbo Mariamu Wangu.Pata burudani.Wikiendi Njema.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

makassybc

Naam. Wikiendi tena. Wakati wa burudani. Wakati wa vikao vya kiti kirefu,familia,harusi,ubatizo,ubarikio,mwali kutolewa ndani nk.Ni muda mwingine wa kupumzisha akili.Hata kama unafanya kazi weekend hii bila shaka utakubaliana nami kwamba hata huko mabarabarani hali huwa shwari. Zile vurugu za foleni,msururu wa watu nk huwa hakuna.Ukiitazama Samora Avenue unaweza kuona kutokea Askari Monument mpaka Clock Tower.Unabisha? Hebu jaribu uone.

Kikubwa wiki hii ni kwamba tumetimiza miaka miwili. Kwa maana hiyo bado tupo kwenye mauzamauza ya kufurahi,kujipongeza na katika semina elekezi ili kuweka mstakabali wa nini kinachofuata. Kwa upande mwingine umemsikia mwenyewe mkuu wa nchi.Anasema habari za uraia wa nchi mbili hazina budi kusubiri. Anasema wasomi wamemshauri kwamba mpango wa kula huku na kule sio mzuri. Mwenyewe akasita kuleta habari za “wivu”. Wakati huo huo mkuu anasema mjenge na kuwekeza “nyumbani”. Nyumbani tena? Sijui wewe unasemaje lakini mimi naona kazi kubwa bado ipo. Washauri wasomi najua wamenielewa. Kama hawajaelewa basi tena.

Turudi kwenye burudani kwani kama ujuavyo leo ni Ijumaa. Ni mambo ya sakayonsa. Mambo ya zilipendwa. Enzi zile ambapo ugonjwa ulikuwa ni mafua tu! Wimbo unaitwa Binadamu Hatosheki kutoka kwao Orchestra Makassy. Bila shaka utakubaliana na kina Mzee Makassy.Binadamu sijui umpe nini aridhike. Hivi kwanini tupo hivyo tulivyo? Kama wanavyoimba; ukimpa jua anataka mvua. Ukimpa mvua anataka jua!Kha. Ukimpenda sana anataka kuchukiwa na ndio maana atakuletea madharau,visa,vituko na visasi.Enewei,wasikilize mwenyewe Orchestra Makassy. Pata burudani na furahia weekend yako.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Subiri kidogo. Kwa sababu wikiendi hii tunaweza kusema ni wikiendi ya BC kwa maana ya kutimiza miaka miwili sidhani kama kuna ubaya kama tukiweka kibao kingine kama zawadi….sikiliza hapo chini;

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

mose-fan-fanbc

Wimbo wa weekend hii nilitakiwa na ilikuwa ni dhamira yangu kuuweka hapa  wikiendi iliyopita. Sababu? Ilikuwa ni Mother’s Day kwa wengi waliopo nchi za magharibi bila kusahau kwamba siku hizi hata sisi hapa Bongo tumeshaambukizwa sijui niseme uzungu au utandawazi. Siku hizi nasi hatupitwi. Halloween tumo, Mother’s Day tumo, Father’s Day tumo,Thanksgiving tumo. Xmas na Pasaka ndio kabisa usiguse kwani hapo utachanganyikiwa nasi. Tuna barafu zetu wenyewe(pamba kwenye miti). Tuna Mbaba Xmas au ukipenda muite Father Christmas.

Sasa kwa sababu sikuuweka wikiendi iliyopita na kwa sababu kwa upande fulani naamini kwamba Mother’s Day ni kila siku, weekend hii tutajimwaya. Wimbo unaitwa Pole Mama na ni wake  Mose Se Sengo “Fan Fan” (pichani) mwanamuziki mahiri kutoka DRC ambaye alizunguka nchi kadhaa za Afrika ikiwemo Tanzania(alicharaza gitaa na Makassy Orchestra). Kama ilivyo kwako wewe, katika wimbo huu Mose Se Sengo anampa pole mama yake na kumshukuru kwa yote. Nani kama mama? Pata burudani na enjoy your weekend. Kumbuka ukiamua kuiloweka,sharti uivalishe…au sio?

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Shukrani: Mike Mhagama…Once a DJ,forever a DJ!

weddingbcWeekend ndio imewadia tena. Kama ulidhani wiki hii ingekuwa kavu kavu nchini Tanzania bila mikikimikiki basi ulikosea.Ilikuwa ni wiki ya “mipasho”. Ilikuwa ni rusha kombora nirushe kombora au kama vile alivyowahi kuimba Prof.Jay ukimwaga ugali mimi namwaga mboga!

Bahati nzuri ni kwamba nadhani watu wazima wamejiona ovyo na kuamua kufuata njia zinazostahili. Mchezo sasa umegeuka kuwa wa kudaiana “vijisenti”. Bila shaka umesikia mmoja kadai fidia ya Tshs Bilioni 10 huku mwingine akidai fidia ya Tsh 1 tu. Kama ingewezekana huenda angedai ile ya mkoloni kabisa iliyokuwa na tundu katikati. Sijui tugange yajayo au bado tuendelee na nguvu ya hoja,uchambuzi nk.

Tuyaache hayo.Leo ni burudani ya kale.Wenyewe mnaziita Zilipendwa. Natamani tungeziita Tunazozipenda kwani ukweli ni kwamba bado nyimbo hizi zina mafundisho kemkem na ni kama zilitungwa jana. Leo tunaye Gwiji Marijan Rajab(RIP). Wimbo unaitwa Ndoa ya Mateso. Binti karudi kwao.Anasema ndoa imemshinda.Mume anamtesa.Pesa zote anamalizia kwenye makuku ya kukaanga akiwa na “vimwana’ wake huko nje wakati familia inakufa kwa njaa.Binti hana msaada wowote,hana ndugu wala jamaa hapo alipo.Kwa masikitiko anauliza kwani kuolewa ni utumwa? Binti anaomba talaka yake.Mjumbe ndie anaombwa kuwa shahidi. Kwa uchungu na aibu anasimulia yaliyokuwa yanamsibu.Anataka kurudi nyumbani kwao kwani anasema hakuzaliwa juu ya miti bali ana kwao.Ana baba na mama. Mateso.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Pata burudani,pata ujumbe na furahia weekend yako. Maisha mafupi haya.

dar-explosionImekuwa ni wiki ngumu kwa watanzania hususani waishio jijini Dar-es-salaam na zaidi waishio maeneo ya Mbagala. Milipuko kadhaa ilitetemesha jiji.Hofu ikatanda. Ikawa mshikemshike Mbagala kwenyewe mpaka katikati ya jiji na maeneo mengine. Wengine wakajua vita nyingine labda ndio imeshawadia.Penye wengi pana mambo mengi. Maneno mitaani nayo yakazidi. Hofu ikawa hofu.

Wananchi kadhaa ambao walikuwa katika siku yao ya kawaida,ya mihangaiko ya kawaida ya maisha wakapoteza maisha. Ama kweli kifo kikija hakipigi hodi! Ndio maana tunaambiwa kila siku kwamba tujiandae. Wengi wengine wakajeruhiwa. Wengi bado wapo mahospitalini.

Vifo vinapotokea au maafa ya namna hii, huwa ni wakati wa simanzi kubwa. Kifo ni kitu cha mwisho ambacho binadamu yeyote anataka kukabiliana nacho.Kinaogopesha. Lakini kifo ni sehemu inayokwenda sambamba kabisa na maisha. Ni sehemu ya maisha na sote tutapitia njia hiyo hiyo.Tunachoweza kufanya ni kutoa pole tu kwa wote walioondokewa na wapendwa wao. Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi! Pole nyingi pia ziwaendee wote waliojeruhiwa.Ni matumaini yetu kwamba Mwenyezi Mungu atawaponya na kukupeni tena afya njema.

Nini kilitokea? Ni ajali au uzembe tu wa mtu au watu fulani? Kama ni uzembe je walioathirika aidha kwa kuumia au kupoteza ndugu,jamaa na marafiki watafidiwa? Je tunavyo vitendea kazi na watendaji wa kutosha kutupatia majibu ya maswali hayo? Hayo ni baadhi ya maswali ambayo serikali ni lazima iyapatie majibu yanayoeleweka,ya wazi bila kificho. Tusipofanya hivyo,kesho bado ni tete. Yanaweza kutokea tena na tena matukio kama hili la wiki hii. Kama hali ile ilitokana na uzembe wa mtu au watu,basi hatua kali zichukuliwe. Ni wakati mwingine muafaka kwa serikali kuonyesha jinsi “inavyowajibika” kwa wapiga kura,walipa kodi na wananchi wake kwa ujumla.

Naam,kwa sababu leo ni Ijumaa na kawaida ni kwamba huwa tunaburudika na zilipendwa na kutokana na hali ya majonzi tuliyonayo,kibao cha Dr.Remmy Ongala cha Kifo ndicho ambacho nadhani ni muafaka. Kimsingi kibao hiki sio cha kuburudisha bali kutusaidia kuungana na wenzetu waliopoteza ndugu,jamaa na marafiki katika maombolezo.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Leo pia ni Mei Mosi. Ni sikukuu ya Wafanyakazi katika sehemu nyingi za ulimwenguni ikiwemo Tanzania yetu. Nachukua nafasi hii kukutakia wewe mfanyakazi na watanzania wote kwa ujumla sikukuu njema.

remmybcMambo vipi?Nadhani nitakuwa sijachelewa sana nikikuuliza ilikuwaje pasaka yako.Ulijichana na kujirarua wapi mwenzangu?Au kutokana na hali ya uchumi ilibidi uwe mpole tu kama mwenzako hapa?

Leo sina maneno mengi.Ni Ijumaa tena na hivyo ni siku ya zilipendwa.Midundo ya leo inatoka kwa Dr.Remmy Ongala & Super Matimila Band.Wimbo unaitwa Nasikitika. 

Tupende tusipende,twende mbele na kurudi nyuma, Dr.Remmy ni miongoni mwa wanamuziki ambao nyimbo zao zilikuwa zina ujumbe mkali sana.Alikuwa anaimba kama masihara hivi lakini ukweli ni kwamba ukiketi chini na kusikiliza ujumbe wake,utaupata kwa makini kabisa. Siku za karibuni nimekuwa namsikiliza sana Dr.Remmy na kwa kweli kila nikimsikiliza nasikitika kwamba mpaka hivi leo sijapata nafasi ya kufanya naye mahojiano kidogo kuhusu muziki,maisha yake na alipo hivi sasa hususani katika dunia ya “ulokole” aliyomo.One day Yes.Pata burudani,weekend njema.

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page